MAISHA YA MKRISTO
Sitawisha Sifa Zinazompendeza Mungu—Unyenyekevu
KWA NINI NI MUHIMU:
Unyenyekevu utafanya tuwe na uhusiano wa karibu na Yehova.—Zb 138:6.
Unyenyekevu unatusaidia tuwe na uhusiano mzuri na wengine.—Flp 2:3, 4
Kiburi kina madhara.—Met 16:18; Eze 28:17.
JINSI YA KUFANYA HIVYO:
Kwa hiari, wafanyie wengine kazi zinazoonekana kuwa za hali ya chini.—Mt 20:25-27
Usiruhusu vipawa au mapendeleo yako yakufanye uwe na kiburi.—Ro 12:3
Ninaweza kuonyeshaje unyenyekevu zaidi?
TAZAMENI VIDEO EPUKA MAMBO YANAYOHARIBU USHIKAMANIFU—KIBURI, KISHA MJIBU MASWALI YAFUATAYO:
Jinsi tunavyoitikia mashauri kunafunua nini kuhusu mtazamo wetu?
Sala inawezaje kutusaidia kusitawisha unyenyekevu?
Tunaweza kuonyesha unyenyekevu katika njia zipi?