Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • mwb17 Oktoba uku. 7
  • Tumia Maisha Yako Kumsifu Yehova!

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Tumia Maisha Yako Kumsifu Yehova!
  • Daftari la Mkutano wa Huduma na Maisha Yetu ya Kikristo—2017
  • Habari Zinazolingana
  • Jifunze Kutokana na Mfano wa Talanta
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2015
  • Kufanya Hesabu Juu ya Matumizi ya Hazina za Kristo
    Usalama Ulimwenguni Pote Chini ya “Mwana-Mfalme wa Amani”
  • Pata Shangwe Katika Mapendeleo Uliyo Nayo
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Funzo)—2021
  • Kielezi cha Talanta
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1990
Pata Habari Zaidi
Daftari la Mkutano wa Huduma na Maisha Yetu ya Kikristo—2017
mwb17 Oktoba uku. 7

MAISHA YA MKRISTO

Tumia Maisha Yako Kumsifu Yehova!

Uhai ni zawadi yenye thamani sana. Jinsi tunavyotumia zawadi hiyo kila siku huonyesha tunaithamini kadiri gani. Tukiwa Mashahidi wa Yehova, tunajitahidi kutumia vipawa na uwezo wetu kumheshimu na kumsifu Yehova, Mpaji-Uhai. (Zb 36:9; Ufu 4:11) Hata hivyo, mahangaiko ya kila siku katika ulimwengu huu mwovu yanaweza kufanya tuache kutanguliza mambo ya kiroho. (Mk 4:​18, 19) Kila mmoja wetu anapaswa kujiuliza: ‘Je, kweli ninampa Yehova kilicho bora? (Ho 14:2) Kazi ninayofanya inaathirije utumishi wangu? Nina miradi gani ya kiroho? Ninaweza kufanya nini ili kupanua utumishi wangu?’ Ikiwa unaona kuna uhitaji wa kufanya maendeleo, sali ili upate msaada wa Yehova halafu ufanye mabadiliko yanayohitajika. Bila shaka, kumsifu Yehova kila siku kunaridhisha na kunatuletea furaha maishani!​—Zb 61:8.

Edgardo Franco akiwa jukwaani; Edgardo Franco akiwa katika huduma

Unatumia vipawa vyako kumsifu nani?

TAZAMENI VIDEO TUMIA VIPAWA VYAKO KUMTUMIKIA YEHOVA, KISHA MJIBU MASWALI YAFUATAYO:

  • Kwa nini si jambo la hekima kutumia vipawa vyako katika ulimwengu wa Shetani? (1Yo 2:17)

  • Wale wanaompa Yehova kilicho bora zaidi wanapata baraka gani?

  • Unaweza kujitolea kutumia vipawa na ustadi wako katika sehemu zipi za utumishi mtakatifu?

MAPENDEKEZO YA IBADA YA FAMILIA:

  • Mhoji mhubiri ambaye amekuwa akimtumikia Yehova kwa miaka mingi, labda katika utumishi wa wakati wote. Amejidhabihu katika njia zipi ili kumpa Yehova kilicho bora? Yehova amembariki katika njia gani?

  • Nenda kwenye JW Broadcasting, tafuta chini ya MAHOJIANO NA MAMBO YALIYOONWA. Utaona na kusikia wengi wakieleza kwa shangwe jinsi ambavyo wametumia maisha yao katika sehemu mbalimbali za utumishi mtakatifu

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki