Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • mwb18 Machi uku. 7
  • “Endeleeni Kukesha”

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • “Endeleeni Kukesha”
  • Daftari la Mkutano wa Huduma na Maisha Yetu ya Kikristo—2018
  • Habari Zinazolingana
  • Je, ‘Utaendelea Kukesha’?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2015
  • Somo Kuhusu Kuwa Macho​—Mabikira
    Yesu—Njia, Kweli, na Uzima
  • Wale Wanawali Wenye Hekima na Wapumbavu
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1990
  • Je, Unatii Onyo?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Funzo)—2024
Pata Habari Zaidi
Daftari la Mkutano wa Huduma na Maisha Yetu ya Kikristo—2018
mwb18 Machi uku. 7
Mabikira kumi wanaotajwa katika mfano wa Yesu

HAZINA ZA NENO LA MUNGU | MATHAYO 25

“Endeleeni Kukesha”

25:1-12

Ingawa Yesu alielekeza mfano wa mabikira kumi kwa wafuasi wake watiwa-mafuta, ujumbe wake muhimu unawahusu Wakristo wote. (w15 3/15 12-16) “Kwa hiyo, endeleeni kukesha kwa sababu hamjui ile siku wala saa.” (Mt 25:13) Je, unaweza kueleza mfano wa Yesu?

  • Bwana harusi (mst. 1)—Yesu

  • Mabikira wenye busara waliojitayarisha (mst. 2)—Wakristo watiwa-mafuta ambao wamejitayarisha kutimiza mgawo wao kwa uaminifu na ambao wanaangaza daima kama mianga hadi mwisho (Flp 2:15)

  • Mwito: “Huyu hapa Bwana harusi!” (mst. 6)—Uthibitisho wa kuwapo kwa Yesu

  • Mabikira wapumbavu (mst. 8)—Wakristo watiwa-mafuta ambao wanaenda kumpokea Bwana harusi lakini hawaendelei kukesha na hawadumishi utimilifu wao

  • Mabikira wenye busara wanakataa kuwapa wenzao mafuta (mst. 9)—Baada ya muhuri wa mwisho, itakuwa kuchelewa sana kwa watiwa-mafuta waaminifu kuwasaidia wale walioacha kuwa waaminifu

  • “Bwana harusi akaja” (mst. 10)—Yesu anakuja karibu na mwisho wa dhiki kuu ili kuhukumu

  • Mabikira wenye busara wanaingia kwenye karamu ya ndoa pamoja na Bwana harusi, na mlango unafungwa (mst. 10)—Yesu anawakusanya watiwa-mafuta waaminifu kwenda mbinguni, lakini wasio waaminifu wanapoteza thawabu yao ya kwenda mbinguni

Mfano huo haufundishi kwamba watiwa-mafuta wengi wataacha kuwa waaminifu na watu wengine wachukue nafasi zao. Badala yake ni onyo kwa kila Mkristo mtiwa-mafuta kwamba ana uwezo wa kuamua kuwa tayari na kukesha au kuwa mpumbavu na kuacha kuwa mwaminifu. Yesu alihimiza hivi: “Iweni tayari.” (Mt 24:44) Hata iwe tuna tumaini gani, Yesu anatazamia kwamba sisi sote tuwe tayari kutumikia kwa uaminifu na kuendelea kukesha.

Ninaonyeshaje kwamba ninaendelea kukesha?

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki