MAISHA YA MKRISTO
Kwa Nini Kutounga Mkono Upande Wowote Ni Muhimu? (Mik 4:2)
Mfano wa Msamaria mwema unatukumbusha kwamba Yehova hana ubaguzi na anataka “tuwatendee watu wote mema”—kutia ndani watu walio na hali ya kiuchumi, rangi, kabila, taifa, au dini tofauti na yetu.—Gal 6:10; Mdo 10:34.
TAZAMENI VIDEO YENYE KICHWA KWA NINI KUTOUNGA MKONO UPANDE WOWOTE NI MUHIMU? (MIK 4:2), KISHA MJIBU MASWALI YAFUATAYO:
Tunajuaje kwamba Mika 4:2 inafafanua mambo yanayotukia kati ya watu wa Mungu leo?
Kutounga mkono upande wowote kunamaanisha nini, na kwa nini ni muhimu?
Andiko la Ufunuo 13:16, 17 linaonyeshaje kwamba mfumo wa kisiasa unajaribu kuathiri kufikiri kwetu na matendo yetu?
Ni mambo gani matatu yanayoweza kudhoofisha azimio letu la kutounga mkono upande wowote?