MAISHA YA MKRISTO
Jinsi Huduma Yetu ya Kutoa Msaada Ilivyowanufaisha Wakristo Katika Visiwa vya Karibea
Leo, kama ilivyokuwa katika karne ya kwanza, tuna pendeleo la kuwaonyesha upendo Wakristo wenzetu ambao wamepatwa na misiba. (Yoh 13:34, 35) Tazameni video Upendo Waonyeshwa Kupitia Kazi ya Kutoa Msaada Visiwani ili kuona jinsi Wakristo walivyoitikia mahitaji ya ndugu na dada zao wanaoishi katika visiwa vya Karibea, kisha mjibu maswali yafuatayo:
Ndugu zetu huko Karibea waliathiriwaje na Kimbunga Irma na Kimbunga Maria?
Yehova amewasaidiaje ndugu zetu katika visiwa vya Karibea kupitia Wakristo wenzao?
Ndugu walioathiriwa walihisije walipojionea upendo mwingi na ukarimu wa ndugu zao?
Ni ndugu na dada wangapi walioshiriki kazi ya kutoa msaada huko Karibea?
Sisi sote tunawezaje kushiriki kazi ya kutoa msaada?
Video hiyo inakufanya uhisije kuhusu kuwa sehemu ya tengenezo hili lenye upendo?