Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • mwb19 Agosti uku. 5
  • Vijana​​—⁠Iweni na “Bidii Katika Matendo Mema”

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Vijana​​—⁠Iweni na “Bidii Katika Matendo Mema”
  • Daftari la Mkutano wa Huduma na Maisha Yetu ya Kikristo—2019
  • Habari Zinazolingana
  • Kutoa Utegemezo kwa Mapainia
    Huduma Yetu ya Ufalme—1992
  • Baraka za Huduma ya Painia
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1997
  • Msifu Yehova Ukiwa Painia
    Daftari la Mkutano wa Huduma na Maisha Yetu ya Kikristo—2020
  • Rekebisho la Matakwa ya Saa kwa Mapainia
    Huduma Yetu ya Ufalme—1999
Pata Habari Zaidi
Daftari la Mkutano wa Huduma na Maisha Yetu ya Kikristo—2019
mwb19 Agosti uku. 5

MAISHA YA MKRISTO

Vijana—Iweni na “Bidii Katika Matendo Mema”

Katika barua aliyomwandikia Tito ambayo iliongozwa na roho ya Mungu, mtume Paulo aliandika kwamba wanaume vijana, kutia ndani Tito, walipaswa kuwa “mfano mzuri wa matendo mema katika mambo yote.” (Tit 2:6, 7) Baadaye katika sura hiyohiyo, alionyesha kwamba watu wa Yehova wamesafishwa ili wawe wenye “bidii katika matendo mema.” (Tit 2:14) Mojawapo ya matendo hayo mema ni kuhubiri na kufundisha kuhusu Ufalme wa Mungu. Ikiwa wewe ni kijana, je, unaweza kutumia nguvu za ujana wako kutumikia ukiwa painia msaidizi au wa kawaida?—Met 20:29.

Ikiwa ungetaka kuwa painia, fanya mipango itakayokusaidia kufikia mradi huo. (Lu 14:28-30) Kwa mfano, utajitegemezaje kifedha ukiwa katika utumishi wa wakati wote? Utatimizaje takwa la saa? Sali kwa Yehova na umweleze kuhusu hali yako. (Zb 37:5) Zungumza kuhusu mipango yako na wazazi wako na wale ambao wamefanikiwa kutumikia wakiwa mapainia. Kisha chukua hatua za kufikia lengo lako. Bila shaka, Yehova atabariki bidii yako katika utumishi wake!

TAZAMENI VIDEO VIJANA WANAOMHESHIMU YEHOVA, KISHA MJIBU MASWALI YAFUATAYO:

  • Vijana fulani wameshinda changamoto zipi ili kutumikia wakiwa mapainia, na walifanya nini ili wafanikiwe?

  • Wazazi wanaweza kuwasaidiaje watoto wao kuwa mapainia wa kawaida?

  • Kwa nini ni muhimu kuwa na ratiba ya kuhubiri?

  • Washiriki wa kutaniko wanaweza kumtiaje moyo na kumsaidia painia?

  • Wale wanaotumikia wakiwa mapainia wanapata baraka zipi?

Dada kijana akizungumza na baba yake kuhusu kufanya upainia; ndugu kijana akiandika ratiba yake; dada painia kijana akiandamana na dada mwingine katika utumishi wa shambani; dada painia kijana akiongoza funzo la Biblia

Ninaweza kufikiaje mradi wa kuwa painia?

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki