Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • mwb19 Septemba uku. 7
  • “Endelea Kuyafikiria Mambo Hayo”

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • “Endelea Kuyafikiria Mambo Hayo”
  • Daftari la Mkutano wa Huduma na Maisha Yetu ya Kikristo—2019
  • Habari Zinazolingana
  • Wafilipi 4:8—“Mambo Yoyote Yaliyo ya Kweli, . . . Endeleeni Kuyafikiria Mambo Hayo”
    Mistari ya Biblia Yafafanuliwa
  • Utimilifu na Mawazo Yako
    Daftari la Mkutano wa Huduma na Maisha Yetu ya Kikristo—2023
  • Kutafakari kwa Moyo Wangu
    ‘Mwimbieni Yehova kwa Shangwe’
  • Tunaweza Kutiaje Wema-adili Katika Imani Yetu?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1993
Pata Habari Zaidi
Daftari la Mkutano wa Huduma na Maisha Yetu ya Kikristo—2019
mwb19 Septemba uku. 7
Ndugu akitumia kompyuta yake usiku na simba anayenguruma, akiwakilisha Shetani, akiwa kando yake

MAISHA YA MKRISTO

“Endelea Kuyafikiria Mambo Hayo”

Mambo gani? Wafilipi 4:8 inasema tufikirie mambo yaliyo ya kweli, ya hangaiko zito, ya uadilifu, safi kiadili, yanayopendeka, yanayosemwa vema, wema wa adili, na yanayostahili sifa. Bila shaka, hilo halimaanishi Mkristo anahitaji kufikiri tu kuhusu mambo ya Biblia kila wakati. Hata hivyo, mambo tunayochagua kufikiria yanapaswa kuwa yenye kupendeza machoni pa Yehova. Hatupaswi kufikiria mambo yatakayofanya iwe vigumu kwetu kudumisha uaminifu kwake.​—Zb 19:14.

Inaweza kuwa vigumu kuepuka mawazo yasiyofaa. Mbali na kupinga mwelekeo wetu usio mkamilifu tunahitaji pia kukabiliana na Shetani, “mungu wa mfumo huu wa mambo.” (2Ko 4:4) Kwa kuwa anadhibiti vyombo vya habari vya ulimwengu huu, mambo mengi yaliyo kwenye televisheni, redio, Intaneti, na yaliyochapishwa ni mapotovu. Tusipoteua kwa uangalifu mambo tunayojaza akilini, kufikiri kwetu kutapotoshwa, na hatimaye mwenendo wetu utaathiriwa.​—Yak 1:14, 15.

TAZAMENI VIDEO YENYE KICHWA EPUKA MAMBO YANAYOHARIBU USHIKAMANIFU—BURUDANI ZISIZOFAA, KISHA MJIBU MASWALI YAFUATAYO:

  • Ndugu akitazama mambo yenye kutiliwa shaka kwenye simu yake usiku sana

    Ndugu huyo alikuwa akitazama nini kwenye simu yake, naye aliathiriwaje?

  • Ndugu akijitoa kwenye tovuti ya mtandao wa kijamii

    Maandiko ya Wagalatia 6:7, 8 na Zaburi 119:37 yalimsaidiaje?

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki