MAISHA YA MKRISTO
“Endelea Kuyafikiria Mambo Hayo”
Mambo gani? Wafilipi 4:8 inasema tufikirie mambo yaliyo ya kweli, ya hangaiko zito, ya uadilifu, safi kiadili, yanayopendeka, yanayosemwa vema, wema wa adili, na yanayostahili sifa. Bila shaka, hilo halimaanishi Mkristo anahitaji kufikiri tu kuhusu mambo ya Biblia kila wakati. Hata hivyo, mambo tunayochagua kufikiria yanapaswa kuwa yenye kupendeza machoni pa Yehova. Hatupaswi kufikiria mambo yatakayofanya iwe vigumu kwetu kudumisha uaminifu kwake.—Zb 19:14.
Inaweza kuwa vigumu kuepuka mawazo yasiyofaa. Mbali na kupinga mwelekeo wetu usio mkamilifu tunahitaji pia kukabiliana na Shetani, “mungu wa mfumo huu wa mambo.” (2Ko 4:4) Kwa kuwa anadhibiti vyombo vya habari vya ulimwengu huu, mambo mengi yaliyo kwenye televisheni, redio, Intaneti, na yaliyochapishwa ni mapotovu. Tusipoteua kwa uangalifu mambo tunayojaza akilini, kufikiri kwetu kutapotoshwa, na hatimaye mwenendo wetu utaathiriwa.—Yak 1:14, 15.
Ndugu huyo alikuwa akitazama nini kwenye simu yake, naye aliathiriwaje?
Maandiko ya Wagalatia 6:7, 8 na Zaburi 119:37 yalimsaidiaje?