MAISHA YA MKRISTO
Utimilifu na Mawazo Yako
Tunaonyesha utimilifu si tu kupitia mambo tunayosema bali pia kupitia mambo tunayofikiria. (Zb 19:14) Hivyo, Biblia inatuhimiza tufikirie mambo yoyote yaliyo ya kweli, ya hangaiko zito, ya uadilifu, safi kiadili, yanayopendeka, yanayosemwa vema, ya wema wa adili, na yanayostahili sifa. (Flp 4:8) Bila shaka, hatuwezi kuzuia kabisa mawazo mabaya yasiingie katika akili zetu. Hata hivyo, kujizuia kunaweza kutusaidia kuondoa wazo baya na kulibadili na wazo linalofaa. Kudumisha utimilifu katika kufikiri kwetu kutatusaidia kudumisha utimilifu katika matendo yetu.—Mk 7:21-23.
Chini ya maandiko yafuatayo, andika aina ya kufikiri ambako tunapaswa kuepuka: