HAZINA ZA NENO LA MUNGU | UFUNUO 7-9
Umati Mkubwa Usioweza Kuhesabiwa Utabarikiwa na Yehova
Kwa nini Yehova anabariki umati mkubwa?
“Wamesimama mbele ya kiti cha ufalme” cha Yehova, wakiunga mkono kabisa enzi kuu ya Yehova
“Wamevaa kanzu nyeupe,” jambo linaloonyesha msimamo wao safi wa uadilifu mbele za Yehova kwa sababu ya imani yao katika dhabihu ya Kristo
Wanamtolea “utumishi mtakatifu mchana na usiku,” wakimwabudu Yehova bila kuacha na kwa jitihada zao zote
Ninapaswa kufanya nini ili niwe sehemu ya umati mkubwa?