HAZINA ZA NENO LA MUNGU | MWANZO 15-17
Kwa Nini Yehova Alibadilisha Majina ya Abramu na Sarai?
Yehova alimwona Abramu kuwa mtu asiye na kosa mbele Zake. Alipokuwa akitoa maelezo ya ziada kuhusu ahadi yake kwa Abramu, Yehova aliwapa Abramu na Sarai majina yenye maana ya kinabii.
Kupatana na majina yao, Abrahamu akawa baba ya mataifa mengi na Sara akawa kwenye ukoo uliotokeza wafalme.
Abrahamu
Baba ya Umati
Sara
Binti ya Mfalme
Hatuwezi kuchagua jina tunalopewa tunapozaliwa. Lakini kama Abrahamu na Sara, tunaweza kujijengea sifa nzuri. Jiulize hivi:
‘Ninaweza kufanya nini ili Yehova anione kuwa mtu asiye na kosa?’
‘Ninajenga jina gani mbele za Yehova?’