MAISHA YA MKRISTO
Jihadhari Usieneze Habari za Uwongo
Leo, habari inaweza kusambazwa kwa mamilioni ya watu upesi sana kupitia machapisho, redio, televisheni, na Intaneti. Wale wanaomwabudu yule “Mungu wa ukweli” hawataki kueneza habari za uwongo, hata bila kujua. (Zb 31:5; Kut 23:1) Uwongo unaosambazwa kwa wengine unaweza kutokeza madhara makubwa. Unapojaribu kuamua ikiwa habari fulani ni ya kweli, jiulize:
‘Je, habari hiyo inatoka kwa chanzo kinachotegemeka?’ Huenda anayesimulia habari hiyo hajui habari zote zinazohusika. Habari hubadilika inaposambazwa kutoka kwa mtu mmoja kwenda kwa mwingine, kwa hiyo uwe mwangalifu ikiwa hujui chanzo halisi cha habari hiyo. Kwa kuwa wale walio na mapendeleo kutanikoni ni vyanzo vinavyoheshimika vya habari, wanapaswa hasa kuwa waangalifu kuhusu kupitisha habari ambayo haijathibitishwa
‘Je, habari hiyo ni porojo?’ Ikiwa inaharibu jina au sifa ya mtu au kikundi fulani, huenda isifae kurudia habari hiyo.—Met 18:8; Flp 4:8
‘Je, habari hiyo inapatana na akili?’ Uwe mwangalifu unaposikiliza hadithi na masimulizi yenye kusisimua
TAZAMENI VIDEO YENYE KICHWA NINAWEZAJE KUACHA KUPIGA POROJO? KISHA MJIBU MASWALI YAFUATAYO:
Kulingana na Methali 12:18, maneno yanaweza kusababisha madhara gani?
Wafilipi 2:4 inatusaidiaje kuwa na mtazamo wenye usawaziko kuhusu kuzungumza kuhusu watu wengine?
Tunapaswa kufanya nini watu wanapoanza kuzungumza kwa kejeli au kwa njia isiyofaa kuwahusu wengine?
Kabla ya kuanza kuzungumza kuhusu wengine, ni maswali gani ambayo tunapaswa kujiuliza?