Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • mwb20 Septemba uku. 3
  • Jihadhari Usieneze Habari za Uwongo

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Jihadhari Usieneze Habari za Uwongo
  • Daftari la Mkutano wa Huduma na Maisha Yetu ya Kikristo—2020
  • Habari Zinazolingana
  • “Mtu Asiye na Uzoefu Huamini Kila Neno”
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2015
  • Habari Nyingi Kupita Kiasi
    Amkeni!—1998
  • Zoeeni Kufanya Mambo Ambayo Mmejifunza
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2002
  • Je, Una Habari Kamili?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Funzo)—2018
Pata Habari Zaidi
Daftari la Mkutano wa Huduma na Maisha Yetu ya Kikristo—2020
mwb20 Septemba uku. 3

MAISHA YA MKRISTO

Jihadhari Usieneze Habari za Uwongo

Mwanamke akishtuliwa na kitu alichoona kwenye simu yake akiwa dukani.

Leo, habari inaweza kusambazwa kwa mamilioni ya watu upesi sana kupitia machapisho, redio, televisheni, na Intaneti. Wale wanaomwabudu yule “Mungu wa ukweli” hawataki kueneza habari za uwongo, hata bila kujua. (Zb 31:5; Kut 23:1) Uwongo unaosambazwa kwa wengine unaweza kutokeza madhara makubwa. Unapojaribu kuamua ikiwa habari fulani ni ya kweli, jiulize:

  • ‘Je, habari hiyo inatoka kwa chanzo kinachotegemeka?’ Huenda anayesimulia habari hiyo hajui habari zote zinazohusika. Habari hubadilika inaposambazwa kutoka kwa mtu mmoja kwenda kwa mwingine, kwa hiyo uwe mwangalifu ikiwa hujui chanzo halisi cha habari hiyo. Kwa kuwa wale walio na mapendeleo kutanikoni ni vyanzo vinavyoheshimika vya habari, wanapaswa hasa kuwa waangalifu kuhusu kupitisha habari ambayo haijathibitishwa

  • ‘Je, habari hiyo ni porojo?’ Ikiwa inaharibu jina au sifa ya mtu au kikundi fulani, huenda isifae kurudia habari hiyo.—Met 18:8; Flp 4:8

  • ‘Je, habari hiyo inapatana na akili?’ Uwe mwangalifu unaposikiliza hadithi na masimulizi yenye kusisimua

TAZAMENI VIDEO YENYE KICHWA NINAWEZAJE KUACHA KUPIGA POROJO? KISHA MJIBU MASWALI YAFUATAYO:

  • Mvulana akiwa amefungwa kwenye ubao unaozunguka visu vikiwa vimemzunguka.

    Kulingana na Methali 12:18, maneno yanaweza kusababisha madhara gani?

  • Kikundi cha watu wakiwa wameweka vichwa pamoja wakipiga porojo.

    Wafilipi 2:4 inatusaidiaje kuwa na mtazamo wenye usawaziko kuhusu kuzungumza kuhusu watu wengine?

  • One man turning his back to another man who is gossiping.

    Tunapaswa kufanya nini watu wanapoanza kuzungumza kwa kejeli au kwa njia isiyofaa kuwahusu wengine?

  • Mwanamume akitazama upande mmoja huku aliye nyuma yake akipiga porojo.

    Kabla ya kuanza kuzungumza kuhusu wengine, ni maswali gani ambayo tunapaswa kujiuliza?

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki