HAZINA ZA NENO LA MUNGU | KUTOKA 23-24
Usiufuate Umati
Onyo ambalo Yehova aliwapa mashahidi na mahakimu katika kesi za kihukumu kwamba wasiyumbishwe na umati kutoa ushahidi wa uwongo au hukumu iliyopotoshwa, linahusika pia katika maeneo mengine maishani. Kila wakati ulimwengu unajaribu kuwasonga Wakristo wafikiri na kutenda kama watu wasiomheshimu Yehova wanavyofanya.—Ro 12:2.
Kwa nini si jambo la hekima kuufuata umati
tunaposikia fununu au porojo ambazo hazijathibitishwa?
tunapochagua mavazi, mitindo ya nywele, au burudani?
tunapofikiri kuhusu au kushughulika na watu ambao rangi, utamaduni, hali ya kiuchumi ni tofauti na yetu?