MAISHA YA MKRISTO
Vijana—Je, Yehova Ndiye Rafiki Yenu wa Karibu Zaidi?
Unapochagua rafiki, ungependa awe na sifa zipi? Huenda ungependa awe mshikamanifu, mwenye fadhili, na mkarimu. Yehova ana sifa hizo zote. (Kut 34:6; Mdo 14:17) Anasikiliza unaposali. Anakusaidia unapohitaji msaada wake. (Zb 18:19, 35) Anasamehe makosa yako. (1Yo 1:9) Yehova ni Rafiki mzuri sana.
Unawezaje kuwa rafiki ya Yehova? Jifunze kumhusu kwa kusoma Neno lake. Mweleze hisia zako. (Zb 62:8; 142:2) Onyesha kwamba unathamini mambo ambayo ni muhimu kwa Yehova, kama vile Mwana wake, Ufalme wake, na ahadi zake za wakati ujao. Waeleze wengine kumhusu. (Kum 32:3) Ukisitawisha urafiki wa karibu na Yehova, atakuwa Rafiki yako milele.—Zb 73:25, 26, 28.
TAZAMENI VIDEO YENYE KICHWA VIJANA—“ONJENI MWONE YA KUWA YEHOVA NI MWEMA,” KISHA MJIBU MASWALI YAFUATAYO:
Unaweza kujitayarishaje ili ujiweke wakfu na kubatizwa?
Wengine kutanikoni wanaweza kukusaidiaje kumtumikia Yehova?
Huduma inaimarishaje uhusiano wako na Yehova?
Urafiki wako na Yehova unaweza kudumu milele!
Ni mapendeleo gani unayoweza kufikia katika utumishi wako kwa Yehova?
Ni nini kinachokuvutia kumhusu Yehova?