Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • mwb21 Mei uku. 7
  • Nidhamu—Wonyesho wa Upendo wa Yehova

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Nidhamu—Wonyesho wa Upendo wa Yehova
  • Daftari la Mkutano wa Huduma na Maisha Yetu ya Kikristo—2021
  • Habari Zinazolingana
  • Kuelewa Kusudi la Nidhamu
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2003
  • Je! Wewe Unaweza, Kukubali Nidhamu?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1986
  • Waonaje Adabu?
    Kupata Faida Zote za Ujana Wako
  • Nidhamu​—Uthibitisho wa Upendo wa Mungu
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Funzo)—2018
Pata Habari Zaidi
Daftari la Mkutano wa Huduma na Maisha Yetu ya Kikristo—2021
mwb21 Mei uku. 7
Wazazi wakiwa wamesimama mlangoni wakilia huku wakimtazama mwana wao asiyetubu ambaye ni mtu mzima akiondoka nyumbani.

MAISHA YA MKRISTO

Nidhamu—Wonyesho wa Upendo wa Yehova

Nidhamu inahusiana hasa na mwongozo na elimu, lakini pia inahusisha kurekebisha na kuadhibu. Yehova hututia nidhamu ili tumwabudu kwa njia inayokubalika. (Ro 12:1; Ebr 12:10, 11) Nyakati nyingine nidhamu inaumiza, lakini inaongoza kwenye uadilifu na baraka. (Met 10:7) Wale wanaotoa nidhamu na wale wanaoipokea wanapaswa kukumbuka mambo gani?

Mtoaji. Wazee, wazazi na wengine, hujitahidi sana kutoa nidhamu kwa fadhili na upendo kama Yehova anavyofanya. (Yer 46:28) Hata nidhamu kali inapaswa kutolewa kulingana na uhitaji na ichochewe na upendo.—Tit 1:13.

Mpokeaji. Hatupaswi kuikataa nidhamu hata ikitolewa kwa njia gani, bali tunapaswa kujaribu kuitumia mara moja. (Met 3:11, 12) Tukiwa wanadamu wasio wakamilifu, sote tunahitaji kutiwa nidhamu. Nidhamu hiyo hutolewa kwa njia mbalimbali. Tunaweza kutiwa nidhamu kupitia mambo tunayosoma katika Biblia au kusikia katika mikutano ya kutaniko. Au nyakati nyingine, wengine huhitaji kutiwa nidhamu na halmashauri ya hukumu. Kukubali nidhamu hatimaye huongoza kwenye uzima.—Met 10:17.

TAZAMENI VIDEO YENYE KICHWA “YEHOVA HUWATIA NIDHAMU WALE ANAOWAPENDA,” KISHA MJIBU MASWALI YAFUATAYO:

  • Picha kutoka kwenye video ‘Yehova Huwatia Nidhamu Wale Anaowapenda.’ Canon akihubiri na wazazi wake alipokuwa mtoto.

    Maisha ya Canon yalianzaje, lakini yalibadilikaje?

  • Picha kutoka kwenye video ‘Yehova Huwatia Nidhamu Wale Anaowapenda.’ Canon akikutana na wazee alipokuwa kijana.

    Yehova alimtiaje nidhamu kwa upendo?

  • Picha kutoka kwenye video ‘Yehova Huwatia Nidhamu Wale Anaowapenda.’ Miaka mingi baadaye, Canon akizungumza na vijana kwenye mkutano wa kutaniko.

    Jifunze kupenda nidhamu kutoka kwa Yehova

    Tunajifunza masomo gani kutokana na kisa chake?

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki