MAISHA YA MKRISTO
Uumbaji Unaimarisha Tumaini Letu Katika Hekima ya Yehova
Je, sikuzote Yehova anajua kinachotufaa? Bila shaka! Ikiwa tunaamini hilo, tunaonyesha tuna hekima tunapofuata mwongozo wake. (Met 16:3, 9) Hata hivyo, mwongozo wake unapotofautiana na kile tunachofikiri, huenda imani yetu katika mwongozo huo ikajaribiwa. Tunaweza kuimarisha tumaini letu katika hekima ya Yehova kwa kutafakari kazi zake za uumbaji.—Met 30:24, 25; Ro 1:20.
TAZAMENI VIDEO YENYE KICHWA JE, NI KAZI YA UBUNI? CHUNGU WANAEPUKAJE MSONGAMANO BARABARANI? KISHA MJIBU MASWALI YAFUATAYO:
Chungu wengi hufanya shughuli gani kila siku?
Chungu huepukaje kuwa na msongamano?
Ni kanuni gani ambazo wanadamu wanaweza kuiga ili kuepuka msongamano?
TAZAMENI VIDEO YENYE KICHWA JE, NI KAZI YA UBUNI? UWEZO WA NYUKI WA KURUKA, KISHA MJIBU MASWALI YAFUATAYO:
Wanadamu hukabili changamoto zipi wanapoendesha ndege ndogo?
Nyuki hufauluje kupaa bila matatizo?
Siku moja wanadamu wanaweza kunufaikaje kutokana na hekima ya kisilika ya nyuki?
Umejionea uthibitisho gani wa hekima ya Yehova katika uumbaji katika eneo lenu?