Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • mwb23 Julai uku. 11
  • Unaweza Kusaidia Familia Yenu Iwe na Shangwe Zaidi

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Unaweza Kusaidia Familia Yenu Iwe na Shangwe Zaidi
  • Daftari la Mkutano wa Huduma na Maisha Yetu ya Kikristo—2023
  • Habari Zinazolingana
  • Shangwe
    Ufahamu wa Kina wa Maandiko
  • Shauri la Mama Lenye Hekima
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2000
  • Jinsi Familia Yako Inavyoweza Kuwa na Furaha
    Biblia Inatufundisha Nini?
  • Nidhamu—Wonyesho wa Upendo wa Yehova
    Daftari la Mkutano wa Huduma na Maisha Yetu ya Kikristo—2021
Pata Habari Zaidi
Daftari la Mkutano wa Huduma na Maisha Yetu ya Kikristo—2023
mwb23 Julai uku. 11
Picha: Picha zimetolewa kwenye video “Sitawisha Shangwe Katika Familia Yako.” 1. Mabinti wawili wanatazama wazazi wao wakifurahia keki. 2. Mabinti wakicheka katika ibada ya familia. 3. Mmoja wa mabinti anaongea na mama yake ambaye amelala kwenye kochi akiwa mgonjwa.

MAISHA YA MKRISTO

Unaweza Kusaidia Familia Yenu Iwe na Shangwe Zaidi

Yehova anataka familia ziwe na furaha. (Zb 127:3-5; Mhu 9:9; 11:9) Hata hivyo, tunaweza kupoteza shangwe yetu kwa sababu ya mikazo ya ulimwengu huu na makosa ya watu wa familia yetu. Kila mtu katika familia anaweza kufanya nini ili kusaidia familia iwe na shangwe zaidi?

Mume anampa mke wake heshima. (1Pe 3:7) Anatumia wakati pamoja naye. Hatazamii mengi kupita kiasi kutoka kwake na anaonyesha kwamba anathamini yote anayofanya kwa ajili yake na kwa ajili ya familia. (Kol 3:15) Anamwonyesha kwa maneno na matendo kwamba anampenda na pia anamsifu.​—Met 31:28, 31.

Mke hutafuta njia za kumuunga mkono mume wake. (Met 31:12) Anajitiisha kwake na kushirikiana naye. (Kol 3:18) Anazungumza naye kwa fadhili, na anazungumza mambo mazuri kumhusu.​—Met 31:26.

Wazazi hutumia muda pamoja na watoto wao. (Kum 6:6, 7) Wanawaambia watoto wao kwamba wanawapenda. (Mt 3:17) Wanapowatia nidhamu wanafanya hivyo kwa upendo na kwa busara.​—Efe 6:4.

Watoto wanawaheshimu na kuwatii wazazi wao. (Met 23:22) Wanawaeleza wazazi wao mambo wanayofikiria na wanayohisi. Wanakubali nidhamu ya wazazi wao na kuwaonyesha heshima.​—Met 19:20.

TAZAMENI VIDEO YENYE KICHWA SITAWISHA SHANGWE KATIKA FAMILIA YAKO, KISHA MJIBU SWALI LIFUATALO:

• Kila mmoja alifanya nini ili kuchangia shangwe katika familia?

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki