MAISHA YA MKRISTO
Wazazi—Wafundisheni Watoto Wenu Jinsi ya Kumfanya Mungu Ashangilie
Yehova anawaona vijana kuwa wenye thamani. Anatambua maendeleo yao ya kiroho na uvumilivu wao. (1Sa 2:26; Lu 2:52) Hata ikiwa wao ni wachanga sana, watoto wanaweza kuufurahisha moyo wa Yehova kwa mwenendo wao mzuri. (Met 27:11) Kupitia tengenezo lake, Yehova ameandaa vifaa bora ambavyo vinawasaidia wazazi kuwafundisha watoto wao kumpenda na kumtii Yehova.
TAZAMENI VIDEO YENYE KICHWA WATOTO—UVUMILIVU WENU UNAMFANYA YEHOVA ASHANGILIE! KISHA MJIBU MASWALI YAFUATAYO:
Yehova amewapa vijana msaada na mwongozo gani kadiri ambavyo miaka imepita?
Leo kuna vifaa gani vya kuwasaidia wazazi?
Ikiwa wewe ni kijana, ni kifaa gani ambacho Yehova ameandaa kilichokunufaisha, na kwa nini?