MAISHA YA MKRISTO
Mchango Wangu kwa Sifa Yetu Nzuri
Watu huona mwenendo wa Mashahidi wa Yehova. (1Ko 4:9) Tunaweza kujiuliza, ‘Je, maneno na matendo yangu yanamletea Yehova utukufu?’ (1Pe 2:12) Kwa kweli tusingependa kufanya jambo lolote ambalo litachafua jina zuri ambalo Mashahidi wa Yehova wamejipatia kwa miaka mingi.—Mhu 10:1.
Katika hali zifuatazo, andika jinsi Mkristo anavyopaswa kutenda na pia uandike kanuni ya Biblia inayoweza kusaidia:
Mtu ambaye si mwamini anakuchambua kwa hasira
Unakosa kudumisha unadhifu wa mavazi, gari, au nyumba yako
Sheria fulani ya eneo lenu inaonekana kuwa si ya haki au ni ngumu kutii
Watafiti wa Idara ya Uandikaji wanachangiaje sifa yetu nzuri?
TAZAMENI VIDEO YENYE KICHWA KUCHOCHEA UPENDO NA HESHIMA KWA AJILI YA KWELI, KISHA MJIBU SWALI LIFUATALO:
Ni nini kinachokuvutia kuhusu jitihada za tengenezo letu za kutayarisha habari sahihi?