Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • wp21 Na. 1 kur. 8-9
  • Kwa Nini Mungu Hasikilizi Baadhi ya Sala?

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Kwa Nini Mungu Hasikilizi Baadhi ya Sala?
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Toleo la Watu wote)—2021
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • “Anayekataa kusikiliza sheria​—hata sala yake inachukiza.”​—Methali 28:9.
  • Mkaribie Mungu Katika Sala
    Biblia Inafundisha Nini Hasa?
  • Je! Mungu Anasikiliza Sala Zako?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1983
  • Zawadi ya Sala
    Biblia Inatufundisha Nini?
  • Namna ya Kupata Msaada kwa Sala
    Unaweza Kuishi Milele Katika Paradiso Duniani
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Toleo la Watu wote)—2021
wp21 Na. 1 kur. 8-9

Kwa Nini Mungu Hasikilizi Baadhi ya Sala?

Baba yetu wa mbinguni, Yehova Mungu, anapenda kusikiliza sala zinazotoka moyoni. Hata hivyo, kuna mambo yanayoweza kumfanya asisikilize sala zetu. Ni mambo gani, na tunapaswa kukumbuka nini tunaposali? Ona baadhi ya miongozo tunayopata kwenye Biblia.

Watu wakiwa kanisani wakisoma sala kwenye vitabu.

“Mnaposali msiseme mambo yaleyale tena na tena.”​—Mathayo 6:7.

Yehova hataki turudie-rudie sala ambazo tumekariri au kuzisoma kutoka kwenye kitabu cha sala. Badala yake, anataka tusali kutoka moyoni. Ungehisije ikiwa una rafiki ambaye anakwambia maneno yaleyale kila siku? Marafiki wa kweli huzungumza waziwazi na kutoka moyoni. Tunaposali kwa maneno yetu wenyewe, tunamweleza Baba yetu wa mbinguni mambo yaliyo moyoni mwetu.

Mwanaume ameangalia juu huku akisugua tiketi ya bahati nasibu.

“Mnapoomba, hampokei kwa sababu mnaomba kwa kusudi baya.”​—Yakobo 4:3.

Tunajua kwamba Mungu hawezi kujibu sala zetu ikiwa tutamwomba mambo ambayo hayampendezi au yasiyofaa. Kwa mfano, je, Yehova anaweza kusikiliza sala ya mcheza-kamari, anayeomba bahati njema ilhali Yehova amekataza waziwazi pupa na kuamini mambo yasiyo ya kweli kama vile, bahati? (Isaya 65:11; Luka 12:15) Bila shaka, hatuwezi kutarajia Yehova ajibu sala kama hizo! Ili Mungu ajibu sala zetu, tunapaswa kuhakikisha kwamba mambo tunayomwomba yanapatana kabisa na kile anachotuambia kwenye Biblia.

Kasisi akiombea wanajeshi.

“Anayekataa kusikiliza sheria​—hata sala yake inachukiza.”​—Methali 28:9.

Katika nyakati za Biblia, Mungu hakusikiliza sala za watu ambao hawakutii sheria zake. (Isaya 1:15, 16) Mungu hajabadilika. (Malaki 3:6) Ikiwa tunataka asikilize sala zetu, ni lazima tujitahidi kutii na kuishi kulingana na sheria zake. Namna gani ikiwa zamani tulifanya makosa fulani? Je, inamaanisha kwamba Yehova hatasikiliza sala zetu kamwe? Bila shaka la! Mungu atatusamehe kwa upendo ikiwa tutaonyesha kweli tunajutia mambo tuliyofanya na tunajitahidi kufanya yote tuwezayo ili kumpendeza.—Matendo 3:19.

“Yule anayemkaribia Mungu lazima aamini kuwa yuko na kwamba yeye huwa mthawabishaji wa wale wanaomtafuta kwa bidii.”​—Waebrania 11:6.

Mwanamke akisoma Biblia.

Hatusali ili tu tuhisi vizuri tunapokuwa na matatizo au mahangaiko maishani. Tunaposali tunaonyesha kwamba tunamwamini Mungu na tunamwabudu yeye. Mtume Yakobo alisema, ikiwa mtu haendelei “kuomba kwa imani, . . . asitarajie kupokea kitu chochote kutoka kwa Yehova.” (Yakobo 1:6, 7) Ili tuwe na imani kwa Mungu, tunahitaji kutenga wakati wa kujifunza Biblia. Kufanya hivyo, kutatusaidia kujua mapenzi yake na kuwa na uhakika kwamba anasikiliza sala zetu.

USIKATE TAMAA!

Ingawa Mungu hasikilizi baadhi ya sala, yeye husikiliza na kujibu sala za mamilioni ya watu wanyoofu. Biblia inataja mambo unayoweza kufanya ili sala zako zimpendeze Mungu. Makala inayofuata itafafanua mambo hayo.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki