Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w21 Januari uku. 31
  • Je, Wajua?

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Je, Wajua?
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Funzo)—2021
  • Habari Zinazolingana
  • Je, Ni Vibaya Kutumia Jina La Mungu?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2008
  • Jina la Mungu Katika Vizazi Vingi
    Jina la Mungu Litakaloendelea Milele
  • Je, Mungu Ana Jina?
    Maswali ya Biblia Yajibiwa
  • Yehova
    Kutoa Sababu kwa Kutumia Maandiko
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Funzo)—2021
w21 Januari uku. 31
Jina la Mungu likiwa limeandikwa kwenye kipande cha jiwe.

Maandishi kwenye jiwe: “Alaaniwe Hagaf mwana wa Hagav na Yahweh Sabaot”

Je, Wajua?

Maandishi fulani ya kale yanaiungaje mkono Biblia?

JIWE lenye maandishi yaliyoandikwa kati ya mwaka wa 700-600 K.W.K. hivi, limehifadhiwa kwenye makumbusho ya Bible Lands Museum huko Jerusalem. Jiwe hilo lilipatikana kwenye pango la kuzikia lililo karibu na Hebroni huko Israeli. Maandishi hayo yanasema: “Alaaniwe Hagaf mwana wa Hagav na Yahweh Sabaot.” Maandishi hayo yanaiungaje mkono Biblia? Yanaonyesha kwamba jina la Mungu Yehova, linaloandikwa YHWH katika herufi za Kiebrania cha kale, lilijulikana sana na kutumiwa katika maisha ya kila siku ya watu wa nyakati za Biblia. Isitoshe, maandishi mengine yanayopatikana katika mapango hayo ya kuzikia yanaonyesha kwamba wale waliotumia mapango hayo kama mahali pa kukutana na kujificha, waliandika mara nyingi jina la Mungu kwenye kuta za mapango hayo, pamoja na majina ya kibinafsi yaliyotia ndani jina la Mungu.

Akizungumzia maandishi hayo, Dakt. Rachel Nabulsi wa Chuo Kikuu cha Georgia alisema hivi: “Kutumiwa tena na tena kwa jina YHWH ni jambo muhimu. . . . Maandishi hayo yanaonyesha umuhimu wa jina YHWH katika maisha ya watu wa Israeli na Yuda.” Jambo hilo linaiunga mkono Biblia, ambamo jina la Mungu, linaloandikwa YHWH katika herufi za Kiebrania, linapatikana mara elfu kadhaa. Mara nyingi majina ya kibinafsi ya watu yalitia ndani jina la Mungu.

Maneno “Yahweh Sabaot,” yaliyoandikwa kwenye kipande hicho cha jiwe, yanamaanisha “Yehova wa majeshi.” Hivyo, inaonekana kwamba katika nyakati za Biblia, watu hawakutumia tu kwa ukawaida jina la Mungu, bali pia msemo “Yehova wa majeshi.” Hilo linaunga mkono pia matumizi ya Biblia ya msemo “Yehova wa majeshi,” unaopatikana mara 283 katika Maandiko ya Kiebrania, hasa katika vitabu vilivyoandikwa na Isaya, Yeremia, na Zekaria.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki