Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w21 Novemba uku. 31
  • Je, Wajua?

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Je, Wajua?
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Funzo)—2021
  • Habari Zinazolingana
  • Kitabu cha Biblia Namba 34—Nahumu
    “Kila Andiko, Lenye Pumzi ya Mungu, Lafaa”
  • Milki Iliyopotea Ambayo Iliwaaibisha Wahakiki wa Biblia
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1993
  • Nahumu—Yaliyomo
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
  • Kitabu Kinachotegemeka—Sehemu ya 2
    Amkeni!—2010
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Funzo)—2021
w21 Novemba uku. 31
Maoni ya mchoraji ya jinsi majengo na minara ya ukumbusho ya Ninawi la kale ilivyokuwa.

Ninawi lilikuwa jiji lenye majengo na minara mikubwa ya ukumbusho

Je, Wajua?

Ni nini kilicholipata jiji la Ninawi baada ya siku za Yona?

BLOGU ya Jumba la Makumbusho la Uingereza iliripoti kwamba kufikia karne ya saba K.W.K., Ashuru ilikuwa milki kubwa zaidi ya ulimwengu, “ikianzia Kipro kwa upande wa magharibi hadi Iran kwa upande wa mashariki, na pindi fulani hata ilitia ndani Misri.” Ninawi, jiji lake kuu, lilikuwa jiji kubwa zaidi duniani. Lilikuwa na minara mikubwa ya ukumbusho, bustani maridadi, makasri ya kifahari, na maktaba kubwa. Maandishi ya ukutani katika jiji la kale la Ninawi yanaonyesha kwamba Mfalme Ashurbanipali, kama wafalme wengine wa Ashuru, alijiita “mfalme wa ulimwengu.” Wakati huo, ilionekana kana kwamba hakuna ambaye angeweza kuishinda Ashuru na Ninawi.

Ramani inayoonyesha mipaka ya Milki ya Ashuru katika karne ya saba K.W.K. Maeneo yaliyoonyeshwa kwenye ramani ni Misri, kisiwa cha Kipro, na Ninawi.

Serikali Kuu ya Ulimwengu ya Ashuru ilikuwa milki kuu zaidi ulimwenguni wakati huo

Hata hivyo, Ashuru ilipokuwa imefikia kilele cha mafanikio, Sefania, nabii wa Yehova, alitabiri hivi: “[Yehova] . . . [ataangamiza] Ashuru, naye atalifanya Ninawi liwe ukiwa, liwe kavu kama jangwa.” Pia, Nahumu, nabii wa Yehova, alitabiri hivi: “Poreni fedha, poreni dhahabu! . . . Jiji liko tupu, liko ukiwa, na limeharibiwa kabisa! . . . Kila mtu atakayekuona atakukimbia na kusema, ‘Jiji la Ninawi limeangamizwa!’” (Sef. 2:13; Nah. 2:9, 10; 3:7) Watu waliposikia unabii huo, huenda walijiuliza hivi: ‘Je, kweli hilo linawezekana? Je, kweli Ashuru yenye nguvu inaweza kushindwa?’ Ni lazima lilionekana kuwa jambo lisilowezekana.

Ninawi likawa jiji lililoachwa ukiwa!

Hata hivyo, lile ambalo halikudhaniwa lilitukia! Kufikia mwishoni mwa karne ya saba K.W.K., Ashuru ilikuwa imeshindwa na Wababiloni na Wamedi. Hatimaye, Ninawi liliachwa ukiwa na kusahaulika! Chapisho lililotolewa na Jumba la Makumbusho ya Sanaa la Jijini New York, lilisema hivi: “Kufikia zile Enzi za Kati, eneo hilo lilikuwa limeachwa ukiwa na kufukiwa, na Ninawi ilikumbukwa tu kupitia Biblia.” Kulingana na Hifadhi ya Mtandaoni ya Biblical Archaeology Society, kufikia mwanzoni mwa miaka ya 1800, “hakuna hata aliyekuwa anajua ikiwa jiji kuu la Ashuru liliwahi kuwepo.” Lakini mwaka wa 1845, mvumbuzi wa vitu vya kale, Austen Henry Layard, alianza kuchimbua eneo la jiji la Ninawi. Magofu yaliyogunduliwa yalithibitisha utukufu wa kale wa jiji la Ninawi.

Kutimia kwa usahihi kwa unabii mbalimbali kuhusu Ninawi kunaimarisha uhakika wetu kwamba unabii wa Biblia kuhusu mwisho wa serikali kuu za leo utatimia pia.​—Dan. 2:44; Ufu. 19:15, 19-21.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki