Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w22 Julai uku. 31
  • Maswali Kutoka kwa Wasomaji

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Maswali Kutoka kwa Wasomaji
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Funzo)—2022
  • Habari Zinazolingana
  • Kweli Huleta, “Si Amani, Bali Upanga”
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Funzo)—2017
  • Unaweza Kupata Furaha Katika Familia Iliyogawanyika
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2012
  • Je, Mungu Hutangulizwa Katika Familia Yako?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1995
  • Jitahidi Kumfikia Mwenzi wa Ndoa Asiye Mwamini
    Huduma Yetu ya Ufalme—2010
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Funzo)—2022
w22 Julai uku. 31

Maswali Kutoka kwa Wasomaji

Yesu alimaanisha nini aliposema: “Msifikiri nilikuja kuleta amani”?

Yesu alitangaza ujumbe wa amani. Hata hivyo, pindi moja aliwaambia hivi mitume wake: “Msifikiri nilikuja kuleta amani duniani, sikuja kuleta amani, bali upanga. Kwa maana nilikuja kuleta mgawanyiko, mtu dhidi ya baba yake, binti dhidi ya mama yake, na binti mkwe dhidi ya mama mkwe wake.” (Mt. 10:34, 35) Yesu alimaanisha nini?

Yesu hakutaka kuwatenganisha washiriki wa familia, lakini alijua kwamba mafundisho yake yangesababisha mgawanyiko katika baadhi ya familia. Basi, wale waliotamani kuwa wanafunzi wa Kristo na kubatizwa, walihitaji kujua matokeo ambayo yangesababishwa na uamuzi wao. Ikiwa wangekabili upinzani kutoka kwa mwenzi asiyeamini au wengine katika familia, huenda ingekuwa vigumu kuendelea kuwa waaminifu kwa mafundisho ya Kristo.

Biblia inawatia moyo Wakristo hivi: “Fanyeni amani na watu wote.” (Rom. 12:18) Lakini mafundisho ya Yesu yanaweza kuwa kama “upanga” katika baadhi ya familia. Inakuwa hivyo mshiriki mmoja wa familia anapokubali mafundisho ya Yesu, lakini wengine wanayakataa au kuyapinga. Katika kisa kama hicho, watu wa ukoo, yaani, watu wa nyumbani mwake, wanakuwa “adui” za yule anayejifunza kweli.—Mt. 10:36.

Mwanamke kijana akitembea kwa uhakika na kumwacha mama yake, ambaye anaonyesha ishara na kumsihi. Mwanamke huyo ameshika kitabu “Furahia Maisha Milele!”

Wanafunzi wa Kristo wanaoishi katika nyumba iliyogawanyika kidini, wakati mwingine wanakabili hali zinazojaribu upendo wao kwa Yehova na Yesu. Kwa mfano, watu wa ukoo wasio waamini wanaweza kuwahimiza washerehekee sikukuu ya kidini. Wanapojaribiwa, wanapaswa kuamua watamfurahisha nani? Yesu alisema: “Yeyote anayempenda baba au mama kuliko anavyonipenda hanistahili.” (Mt. 10:37) Bila shaka, Yesu hakuwa akisema kwamba ili wanafunzi wake wapate kibali chake walipaswa kupunguza upendo wao kwa wazazi wao. Badala yake, alikuwa akikazia kuhusu kutanguliza mambo muhimu. Ikiwa washiriki wa familia yetu wasio waamini wanapinga jitihada zetu za kumwabudu Yehova, tunaendelea kuwapenda, lakini tunakumbuka kwamba tunapaswa kutanguliza upendo wetu kwa Mungu.

Bila shaka, upinzani kutoka kwa watu wa familia unaumiza sana. Lakini wanafunzi wa Yesu wanakumbuka maneno haya aliyosema: “Yeyote asiyechukua mti wake wa mateso na kunifuata hanistahili.” (Mt. 10:38) Hilo linamaanisha Wakristo wanaona upinzani kutoka kwa watu wa familia kuwa sehemu ya mateso ambayo wanafunzi wa Kristo wanakubali kwa hiari. Wakati huohuo, wanatumaini kwamba mwenendo wao mzuri utawachochea watu wao wa familia wasio waamini wabadili maoni yao na wachochewe kujifunza Biblia.​—1 Pet. 3:1, 2.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki