Je, Unakumbuka?
Je, umesoma kwa makini matoleo ya Mnara wa Mlinzi ya mwaka huu? Ona ikiwa unaweza kujibu maswali yafuatayo:
Tutathawabishwaje ikiwa tutatumia muda kuzungumza, kumsikiliza, na kufikiria kumhusu Yehova?
Tutafanya maamuzi bora, tutakuwa walimu bora, tutakuwa na imani yenye nguvu zaidi, na upendo wetu kwa Yehova utaongezeka.—w22.01, uku. 30-31.
Tutanufaikaje ikiwa tutajifunza kumtumaini Yehova na wawakilishi wake?
Sasa ndio wakati wa kujifunza kutumaini njia ya Yehova ya kufanya mambo kwa kutotilia shaka mwongozo na maamuzi ya wazee wa kutaniko. Dhiki kuu itakapoanza, tutakuwa tayari kutii hata tukipokea maagizo ambayo yatatushangaza au kuonekana kwamba hayapatani na akili.—w22.02, uku. 4-6.
Malaika alimaanisha nini alipomwambia Zekaria kuhusu “timazi mkononi mwa [Gavana] Zerubabeli”? (Zek. 4:8-10)
Maono hayo yaliwahakikishia watu wa Mungu kwamba hekalu lisilo la kifahari lililokuwa likijengwa lingekamilishwa na kutimiza viwango vya Yehova.—w22.03, uku. 16-17.
Tunawezaje kuwa “mfano mzuri . . . katika kusema”? (1 Tim. 4:12)
Tunazungumza kwa fadhili na kwa heshima katika huduma, tunaimba kwa moyo wote, tunatoa maelezo kwa ukawaida mikutanoni, na tunasema ukweli na kuwajenga wengine, huku tukiepuka matusi.—w22.04, uku. 6-9.
Kwa nini sifa za wanyama wanne wa mwituni (yaani, falme) zinazotajwa katika Danieli sura ya 7 zinaunganishwa na kuwa mnyama mmoja wa mwituni kama inavyofafanuliwa kwenye Ufunuo 13:1, 2?
Mnyama wa mwituni anayefafanuliwa kwenye Ufunuo 13 hawakilishi ufalme mmoja hususa, kama vile Roma. Badala yake, anawakilisha serikali zote ambazo zimewatawala wanadamu.—w22.05, uku. 9.
Ni njia gani kuu ya kuonyesha kwamba tuna uhakika katika haki ya Mungu?
Ikiwa mtu fulani ametutukana, ametukosea, au kututendea dhambi, tunajitahidi kuacha hasira na kinyongo, huku tukiacha mambo mikononi mwa Yehova. Ataondoa madhara yote yaliyosababishwa na dhambi.—w22.06, uku. 10-11.
Ndugu anayetoa sala mkutanoni anapaswa kukumbuka nini?
Sala haipaswi kutumiwa kulishauri kutaniko au kutoa matangazo. Hasa mwanzoni mwa mkutano, hatuhitaji kutumia “maneno mengi.” (Mt. 6:7)—w22.07, uku. 24-25.
Ni kwa njia gani “wale waliozoea kutenda maovu” watapata “ufufuo wa hukumu”? (Yoh. 5:29)
Hawatapata hukumu isiyofaa kwa kutegemea maisha yao ya zamani. Watapimwa na kuchunguzwa kwa msingi wa mtazamo na matendo yao baada ya kufufuliwa.—w22.09, uku. 18.
Ndugu J. F. Rutherford alitoa himizo gani lenye kusisimua kwenye kusanyiko mnamo Septemba 1922?
Kwenye kusanyiko huko Cedar Point, Ohio, Marekani, alitanganza hivi: “Mfalme anatawala! Ninyi ndio mawakala wa kumtangaza. Kwa hiyo, mtangazeni, mtangazeni, mtangazeni, Mfalme na Ufalme wake!”—w22.10, uku. 3-5.
Isaya sura ya 30 inataja njia gani tatu ambazo Yehova hutusaidia kuvumilia?
Sura hii inaonyesha kwamba (1) anasikiliza na kujibu sala zetu, (2) anatuandalia mwongozo, na (3) anatubariki sasa na pia atatubariki wakati ujao.—w22.11, uku. 9.
Kwa nini tunaweza kufikia mkataa kwamba maneno ya Zaburi 37:10, 11, 29 yalitimizwa zamani na pia yatatimizwa wakati ujao?
Maneno ya Daudi yanafafanua vizuri baraka ambazo zilikuwepo katika Israeli, kama vile wakati wa utawala wa Sulemani. Yesu alizungumzia paradiso ya wakati ujao na akanukuu mstari wa 11. (Mt. 5:5; Luka 23:43)—w22.12, uku. 8-10, 14.