Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w23 Agosti uku. 18-uku. 19 fu. 3
  • Maswali Kutoka Kwa Wasomaji

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Maswali Kutoka Kwa Wasomaji
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Funzo)—2023
  • Habari Zinazolingana
  • “Jina Lako na Litakaswe”
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Funzo)—2020
  • Kwa Nini Ni Lazima Tujue Jina la Mungu
    Jina la Mungu Litakaloendelea Milele
  • Yehova Analikweza Jina Lake
    Ufalme wa Mungu Unatawala!
  • Jina la Yehova Linapaswa Kuwa na Umuhimu Gani Kwetu?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Funzo)—2025
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Funzo)—2023
w23 Agosti uku. 18-uku. 19 fu. 3
Malaika mbinguni na wanadamu katika Paradiso duniani wakimwabudu Yehova kwa shangwe na kulisifu gari lake la kimbingu.

Shetani amelichongea jina la Mungu tangu uasi ulipotokea katika bustani ya Edeni

Maswali Kutoka Kwa Wasomaji

Makala yenye kichwa “Jina Lako na Litakaswe” katika gazeti la Mnara wa Mlinzi la Juni 2020, ilifafanuaje uelewaji wetu kuhusu jina la Yehova na enzi yake kuu?

Katika makala hiyo, tulijifunza kwamba kihalisi kuna suala moja tu ambalo linawakabili viumbe wote wenye akili: kutakaswa kwa jina kuu la Yehova. Suala la enzi kuu—kwamba njia ya Yehova ya kutawala ndiyo bora—ni mojawapo ya sehemu za suala hilo moja kuu. Vivyo hivyo, suala la utimilifu wa wanadamu ni sehemu nyingine ya suala hilo moja kuu.

Kwa nini sasa tunakazia kwamba suala kuu zaidi linahusiana na jina la Yehova na kutakaswa kwa jina hilo? Acheni tuchunguze sababu tatu.

Nyoka akizungumza na Hawa.

Yehova atafanya jina lake litukuzwe kwa umilele wote

Kwanza, Shetani alishambulia jina la Yehova, au sifa yake, katika bustani ya Edeni. Swali la ujanja la Shetani kwa Hawa lilitokeza wazo la kwamba Yehova ni Mungu asiye na ukarimu, ambaye anawawekea wale walio chini ya utawala wake sheria zisizo na usawaziko. Kisha, Shetani akapinga moja kwa moja maneno ya Yehova, na hivyo akadai kwamba Mungu ni mwongo. Kwa hiyo, alilichongea jina la Yehova. Akawa “Ibilisi,” jina linalomaanisha “mchongezi.” (Yoh. 8:44) Kwa sababu Hawa aliamini uwongo wa Shetani, alikosa kumtii Mungu, na akaasi dhidi ya enzi yake kuu. (Mwa. 3:1-6) Kufikia leo, Shetani anaendelea kulichongea jina la Mungu, akieneza uwongo kumhusu Yehova mwenyewe. Ni rahisi zaidi kwa wale wanaoamini uwongo huo kukosa kumtii Yehova. Basi, kwa watu wa Mungu, uchongezi dhidi ya jina takatifu la Yehova ndio ukosefu mkubwa zaidi wa haki. Uchongezi huo ndio chanzo kikuu cha matatizo na uovu wote ulimwenguni.

Pili, ili kuwanufaisha viumbe wote, Yehova ameazimia kulitetea jina lake, na hivyo kuliondolea kila suto. Hilo ndilo jambo muhimu zaidi kwa Yehova. Ndiyo sababu anasema: “Kwa hakika nitalitakasa jina langu kuu.” (Eze. 36:23) Na Yesu alionyesha wazi jambo ambalo linapaswa kuwa muhimu zaidi katika sala zote za watumishi waaminifu wa Yehova aliposema hivi: “Jina lako na litakaswe.” (Mt. 6:9) Biblia inakazia tena na tena umuhimu wa kulitukuza jina la Yehova. Fikiria mifano michache: “Mpeni Yehova utukufu ambao jina lake linastahili.” (1 Nya. 16:29; Zab. 96:8) “Liimbieni sifa jina lake tukufu.” (Zab. 66:2) “Nitalitukuza jina lako milele.” (Zab. 86:12) Pindi moja ambayo Yehova alizungumza kutoka mbinguni, ilikuwa katika hekalu huko Yerusalemu, wakati Yesu alisema hivi: “Baba, litukuze jina lako.” Kisha Yehova akajibu hivi: “Nimelitukuza nami nitalitukuza tena.”​—Yoh. 12:28.a

Tatu, sikuzote kusudi la Yehova linahusiana na jina lake, au sifa yake. Fikiria jambo hili: Baada ya jaribu la mwisho litakalotokea baada ya Utawala wa Miaka Elfu Moja wa Kristo, ni nini kitakachofuata? Je, viumbe wenye akili wataendelea kuwa na mgawanyiko kuhusu lile suala kuu, yaani, kutakaswa kwa jina la Yehova? Ili kutusaidia kujibu swali hilo, kumbuka yale mambo mawili yanayohusiana na suala hilo kuu—utimilifu wa wanadamu na suala la enzi kuu ya ulimwenguni pote. Je, wanadamu ambao watakuwa wamethibitika kuwa waaminifu wataendelea kukabili changamoto ya kudumisha utimilifu wao? Hapana. Watakuwa wakamilifu na watakuwa wamejaribiwa kikamili. Watakuwa wamepokea uzima wa milele. Je, suala la enzi kuu ya ulimwenguni pote, litaendelea kuzungumziwa, au hata kusababisha migawanyiko kati ya viumbe wenye akili? Hapana. Njia ya Yehova ya kutawala itakuwa imethibitishwa kuwa bora kabisa. Namna gani kuhusu jina la Yehova?

Wakati huo, jina la Yehova litakuwa limetakaswa kikamili, na kuondolewa kabisa kila suto. Hata hivyo, jina hilo litaendelea kuwa jambo muhimu zaidi kwa watumishi wote waaminifu wa Yehova mbinguni na duniani. Kwa nini? Kwa sababu watamwona Yehova akiendelea kufanya mambo yenye kustaajabisha. Fikiria jambo hili: Kwa kuwa Yesu, kwa unyenyekevu, atarudisha utawala wote kwa Yehova, Mungu atakuwa “vitu vyote kwa kila mtu.” (1 Kor. 15:28) Baada ya hapo, wanadamu wote duniani, watafurahia “uhuru wenye utukufu wa watoto wa Mungu.” (Rom. 8:21) Na Yehova atakuwa ametimiza kikamili kusudi lake la muda mrefu la kuunganisha viumbe wote wenye akili mbinguni na duniani, katika familia moja kubwa yenye muungano.​—Efe. 1:10.

Mambo hayo yote yatakuwa na matokeo gani kwa familia ya Yehova mbinguni na duniani? Kwa hakika, tutatamani sana kuendelea kulisifu jina maridadi la Yehova. Mtunga zaburi aliongozwa na roho takatifu kuandika hivi: “Na asifiwe Yehova Mungu . . . Jina lake tukufu na lisifiwe milele.” (Zab. 72:18, 19) Kwa umilele wote, tutaendelea kupata sababu mpya na zenye kusisimua za kufanya hivyo.

Kwa hakika, jina la Yehova linawakilisha kila jambo linalomhusu. Tunapofikiria kuhusu jina la Yehova, tunakumbuka hasa upendo wake. (1 Yoh. 4:8) Sikuzote tutakumbuka kwamba Yehova alituumba akichochewa na upendo, aliandaa dhabihu ya fidia kutokana na upendo, na kwamba alithibitisha kuwa njia yake ya kutawala ni ya uadilifu akichochewa na upendo. Lakini tutaendelea kuona jinsi Yehova anavyoonyesha upendo wake mwingi kuelekea uumbaji wake. Kwa umilele wote, tutachochewa kuendelea kumkaribia zaidi akiwa Baba yetu na kuliimbia sifa jina lake tukufu.​—Zab. 73:28.

a Pia, Biblia inaonyesha kwamba Yehova hutenda “kwa ajili ya jina lake.” Kwa mfano, anawaongoza watu wake, anawasaidia, anawakomboa, na kuwahifadhi hai—yote hayo kwa ajili ya jina lake kuu, Yehova.​—Zab. 23:3; 31:3; 79:9; 106:8; 143:11.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki