Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • wp24 Na. 1 kur. 6-9
  • Mema na Mabaya: Biblia​—⁠Mwongozo Unaotegemeka

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Mema na Mabaya: Biblia​—⁠Mwongozo Unaotegemeka
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Toleo la Watu wote)—2024
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • MWONGOZO TUNAOHITAJI
  • BIBLIA INAFUNUA MWONGOZO WA MUNGU
  • Je, Viwango vya Biblia Kuhusu Mema na Mabaya Bado Vinafaa?
    Habari Zaidi
  • Msaada Zaidi Kwa Ajili ya Familia
    Amkeni!—2018
  • Je, Kuna Mwongozo Unaotegemeka wa Kuwa na Maisha Bora ya Wakati Ujao?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Toleo la Watu wote)—2021
  • Mema na Mabaya: Uamuzi Unaopaswa Kufanya
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Toleo la Watu wote)—2024
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Toleo la Watu wote)—2024
wp24 Na. 1 kur. 6-9

Mema na Mabaya: Biblia—Mwongozo Unaotegemeka

Hatuwezi kuwa na uhakika kwamba maamuzi yetu yatakuwa na matokeo mazuri ikiwa tunategemea tu hisia zetu na za wengine. Biblia inatueleza sababu. Isitoshe, inatupatia mwongozo unaotegemeka kuhusu maadili na hilo linatuwezesha kuwa na maisha yenye furaha na yenye kuridhisha.

MWONGOZO TUNAOHITAJI

Katika Biblia, Yehovaa Mungu anasema kwamba wanadamu wanahitaji mwongozo wake kwa sababu hawana uwezo wa kujiongoza. (Yeremia 10:23) Hiyo ndiyo sababu ametupatia mwongozo katika Biblia. Anawapenda wanadamu na hataki tufanye maamuzi mabaya yatakayotuumiza na kufanya maisha yetu yawe magumu. (Kumbukumbu la Torati 5:29; 1 Yohana 4:8) Zaidi ya hilo, yeye ni Muumba wetu na ana hekima na ujuzi unaohitajika ili kutupatia ushauri bora zaidi. (Zaburi 100:3; 104:24) Hata hivyo, Mungu hawalazimishi watu wafuate viwango vyake.

Yehova aliwapatia mwanamume na mwanamke wa kwanza, Adamu na Hawa, kila kitu walichohitaji ili kuwa na furaha ya kweli. (Mwanzo 1:​28, 29; 2:​8, 15) Aliwapatia pia maagizo rahisi ambayo alitarajia wayatii. Hata hivyo, aliwaruhusu wajiamulie ikiwa watafuata maagizo hayo au la. (Mwanzo 2:​9, 16, 17) Kwa kuhuzunisha, Adamu na Hawa walichagua kufuata viwango vyao wenyewe badala ya viwango vya Mungu. (Mwanzo 3:6) Matokeo yalikuwaje? Je, wanadamu wamepata furaha kwa kujiamulia lililo jema au baya? Hapana. Historia ya wanadamu imethibitisha kwamba kupuuza viwango vya Mungu hakuleti amani na furaha ya kudumu.—Mhubiri 8:9.

Biblia inatupatia mwongozo tunaohitaji ili kufanya maamuzi yenye hekima licha ya malezi yetu. (2 Timotheo 3:​16, 17; ona sanduku “Kitabu kwa Ajili ya Watu Wote.”) Ona jinsi Biblia inavyofanya hivyo.

Jifunze kwa nini Biblia inastahili kuitwa “neno la Mungu.”—1 Wathesalonike 2:13. Tazama video Ni Nani Aliyeitunga Biblia? kwenye jw.org.

KITABU KWA AJILI YA WATU WOTE

Tungetazamia Muumba mwenye hekima na upendo ahakikishe kwamba watu wote wanaweza kupata ushauri kutoka kwake. Fikiria mambo haya kuhusu Biblia:

Watu wa mataifa mbalimbali wakisoma Biblia. Biblia kadhaa zilizochapishwa na za kielektroni zinaonekana.
  • 3,500+ Idadi ya lugha ambazo Biblia inapatikana angalau kwa sehemu, Biblia ndicho kitabu kilichotafsiriwa katika lugha nyingi zaidi.

  • 5,000,000,000+ Idadi ya nakala za Biblia zilizochapishwa, Biblia ndicho kitabu kilichosambazwa kwa wingi zaidi katika historia.

Biblia haitukuzi jamii, taifa, kabila, au utamaduni mmoja zaidi ya mwingine. Kwa kweli ni kitabu kwa ajili ya watu wote.

Soma Biblia kwenye mtandao (inapatikana katika lugha zaidi ya 250) kwenye jw.org

Mwanamume akitumia kidole chake kufuatisha maandishi anayosoma katika Biblia.

KWA NINI WENGINE HUIPUUZA BIBLIA

Baadhi ya watu hudai kwamba Biblia si chanzo kizuri cha mwongozo. Huenda wakatoa vipingamizi vifuatavyo.

Kipingamizi: “Biblia inajipinga yenyewe.”

Ukweli: Huenda mistari michache ikaonekana kwamba inapingana, hata hivyo, ukizingatia muktadha, mambo ambayo yamethibitishwa na historia, desturi, maoni ya mwandikaji na mambo mengine utagundua kwamba mistari hiyo inapatana.

Ili kupata mifano hususa, soma makala “Je, Biblia Inajipinga Yenyewe?” kwenye jw.org.

Kipingamizi: “Watu wanaodai kwamba wanafuata Biblia hufanya mambo mabaya, kwa hiyo haitoi mwongozo mzuri.”

Ukweli: Biblia haipaswi kulaumiwa kwa sababu ya matendo mabaya ya wale wanaokataa kutumia mafundisho yake. Biblia ilitabiri kwamba watu wengi kutia ndani viongozi wa kidini wanaodai kuifuata Biblia, wangetenda tofauti na inachosema. Inasema pia kwamba kwa sababu ya watu hao mafundisho ya Biblia ‘yangetukanwa.’—2 Petro 2:​1, 2.

Ili kupata mfano wa jinsi ambavyo viongozi wengi wa kidini wametenda tofauti na mambo ambayo Biblia inafundisha, soma makala “Je, Dini Ni Biashara?” kwenye jw.org.

Kipingamizi: “Biblia inawachochea watu kuwabagua wengine.”

Ukweli: Biblia inatutia moyo tuwatendee wengine kwa heshima. Haiungi mkono. . .

  • kujiona kuwa bora kuliko wengine.—Wafilipi 2:3.

  • kuwavunjia heshima watu wenye maadili au imani tofauti na yetu.—1 Petro 2:17.

  • kuwalazimisha wengine wakubali maoni yetu.—Mathayo 10:14.

Biblia inaonyesha kwamba sikuzote Mungu huwatendea watu kwa fadhili na haki na anataka sisi pia tufanye hivyo.—Waroma 9:14.

Ili kupata habari zaidi, soma makala “Jinsi Biblia Inavyoweza Kukusaidia Kuwa Mstahimilivu” kwenye jw.org.

BIBLIA INAFUNUA MWONGOZO WA MUNGU

Biblia ina habari sahihi kuhusu jinsi ambavyo Yehova amekuwa akishughulika na wanadamu. Habari zilizomo zinatusaidia kuelewa mambo ambayo Mungu anaona kuwa mema au mabaya na mambo anayoona kuwa yenye kunufaisha au yenye madhara. (Zaburi 19:​7, 11) Isitoshe, katika Biblia tunaweza kujifunza kanuni ambazo zinatusaidia kufanya maamuzi yenye hekima maishani.

Kwa mfano, fikiria ushauri unaopatikana kwenye Methali 13:20: “Anayetembea na wenye hekima atakuwa na hekima, lakini anayeshirikiana na wapumbavu ataumia.” Maneno hayo ni ya kweli leo kama yalivyokuwa zamani pia. Biblia ina kanuni nyingi zinazotusaidia. —Ona sanduku “Ushauri wa Biblia Usiopitwa na Wakati.”

Huenda ukajiuliza, ‘Ninawezaje kuwa na uhakika kwamba ushauri wa Biblia unaweza kunisaidia leo?’ Makala inayofuata itakuwa na mifano halisi maishani.

a Yehova ni jina la kibinafsi la Mungu.—Zaburi 83:18.

USHAURI WA BIBLIA USIOPITWA NA WAKATI

Ingawa Biblia ilikamilika miaka 2,000 iliyopita, bado ushauri wake unatumika leo. Wanadamu hawajabadilika, bado wanatafuta maisha yenye furaha na yanayoridhisha. (Mhubiri 1:9) Ushauri wa Biblia usiopitwa na wakati unaweza kutusaidia kufikia lengo hilo.

Unyoofu

  • “Tunataka kujiendesha kwa unyoofu katika mambo yote.”—Waebrania 13:18.

  • “Mwizi asiibe tena; badala yake afanye kazi kwa bidii.”—Waefeso 4:28.

Mahusiano

  • “Kila mmoja na aendelee kutafuta, si faida yake mwenyewe, bali faida ya yule mtu mwingine.”—1 Wakorintho 10:24.

  • “Endeleeni kuvumiliana na kusameheana kwa hiari.”—Wakolosai 3:13.

Kufanya Maamuzi

  • “Mjinga huamini kila neno, lakini mwerevu hutafakari kila hatua.”—Methali 14:15.

  • “Mtu mwerevu huona hatari na kujificha, lakini wajinga husonga mbele na kupata madhara.”—Methali 22:3.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki