Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • wp25 Na. 1 uku. 3
  • Madhara ya Vita

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Madhara ya Vita
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Toleo la Watu wote)—2025
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • WANAJESHI
  • RAIA
  • Kutafuta Amani Licha ya Vita na Ukatili
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Toleo la Watu wote)—2025
  • Vita Nchini Ukrainia Vyaingia Mwaka wa Pili—Biblia Inatoa Tumaini Gani?
    Habari Zaidi
  • Matrilioni Yatumiwa Katika Vita—Gharama Halisi Ni Ipi?
    Habari Zaidi
  • Jinsi Vita na Ukatili Vinavyotuathiri Sisi Sote
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Toleo la Watu wote)—2025
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Toleo la Watu wote)—2025
wp25 Na. 1 uku. 3
Mkusanyo wa picha: 1. Picha iliyochanwa ikionyesha sehemu ya juu ya uso wa mwanajeshi. 2. Picha iliyochanwa ikionyesha sehemu ya juu ya uso wa mwanamke mwenye umri mkubwa.

Madhara ya Vita

Vita na ukatili ni moja kati ya mambo yanayosababisha maumivu makali sana kwa watu. Wanajeshi na raia wengi walioathiriwa na vita wanajua madhara yanayosababishwa na vita.

WANAJESHI

“Mara nyingi, unaona watu waliokuzunguka wakiuawa au kujeruhiwa vibaya. Kila mara unahofia usalama wako.”—Gary, Uingereza.

“Nilipigwa risasi mgongoni na usoni, na niliona watu wengi wakiuawa, kutia ndani watoto na wazee. Vita inafanya moyo wako kuwa mgumu.”—Wilmar, Kolombia.

“Mtu anapopigwa risasi mbele yako, ni vigumu sana kusahau jambo hilo. Akilini mwako unaendelea kusikia kelele za mtu huyo akipigania uhai wake. Huwezi kamwe kumsahau mtu huyo.”—Zafirah, Marekani.

RAIA

“Nilihisi kwamba nisingeweza kuwa na furaha tena. Unahofia uhai wako, lakini unahofia hata zaidi uhai wa familia yako na marafiki.”—Oleksandra, Ukrainia.

“Inaogopesha sana kusimama kwenye foleni kwa ajili ya chakula kuanzia saa 8:00 usiku hadi saa 5:00 usiku, ukihofia kwamba utapigwa risasi.”—Daler, Tajikistan.

“Vita vilisababisha wazazi wangu wauawe. Nilibaki nikiwa yatima bila mtu wa kunifariji au wa kunitunza.”—Marie, Rwanda.

Licha ya matokeo mabaya ya vita, watu wanaotajwa hapo juu wamepata amani. Zaidi ya hilo, wana uhakika kwamba vita na ukatili vitakwisha hivi karibuni. Toleo hili la Mnara wa Mlinzi litatumia Biblia kueleza jinsi jambo hilo litakavyotukia.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki