DOKEZO LA KUJIFUNZA
Jinsi ya Kukumbuka Maandiko
Je, ni vigumu kwako mara nyingine kukumbuka mstari wa Biblia unaoupenda zaidi? Huenda ni andiko ambalo linakufariji, linakusaidia kushinda mawazo yasiyofaa, au ambalo ungependa kushiriki na mtu mwingine. (Zab. 119:11, 111) Fikiria mapendekezo haya yanayoweza kukusaidia kukumbuka maandiko.
Tumia sehemu ya kuongeza tagi kwenye programu ya JW Library®. Unda tagi yenye kichwa “Maandiko Ninayopenda Zaidi,” na hifadhi katika sehemu hiyo maandiko yoyote ambayo unataka kukumbuka.
Bandika andiko katika sehemu ambayo unaweza kuiona. Andika andiko ambalo ungependa kukumbuka kwenye karatasi, na kuibandika mahali ambapo utaiona mara nyingi. Baadhi ya watu hulibandika andiko kwenye kioo, wengine kwenye mlango wa friji. Wengine hupiga picha andiko hilo na kuiweka picha hiyo kwenye skrini ya kompyuta au ya kifaa cha mkononi.
Tengeneza na utumie kadi za kukusaidia kukumbuka. Upande mmoja wa kadi andika jina la kitabu cha Biblia, sura, na mstari na upande mwingine andika maneno ya andiko hilo. Kisha tazama upande ulioandika kitabu cha Biblia na ujaribu kunukuu andiko hilo au tazama upande wenye maneno ya andiko na ujaribu kukumbuka andiko limetoka katika kitabu gani.