DOKEZO LA KUJIFUNZA
Jifunze Ukiwa na Lengo la Kushiriki na Wengine Mambo Uliyojifunza
Vipindi vya kujifunza vinaweza kutuburudisha, lakini tunaweza kuburudika hata zaidi tunaposhiriki na wengine hazina za kiroho zenye kutia moyo tunazopata. Methali 11:25 inasema hivi: “Yule anayewaburudisha wengine yeye mwenyewe ataburudishwa.”
Kushiriki na wengine mambo tuliyojifunza, kunaweza kutusaidia kukumbuka kwa urahisi zaidi mambo tuliyojifunza na kuongeza kina cha uelewaji wetu. Na kwa sababu mambo hayo yanaweza kuwanufaisha wengine, tunafurahia kushiriki hazina hizo pamoja nao.—Mdo. 20:35.
Jaribu kufanya hivi: Katika juma linalofuata, jaribu kutafuta nafasi ya kushiriki na mtu mwingine mambo uliyojifunza. Unaweza kufanya hivyo na mtu wa familia, mtu katika kutaniko lenu, mfanyakazi mwenzako, mwanafunzi mwenzako, jirani yako, au mtu utakayekutana naye katika huduma ya shambani. Jaribu kuzungumzia habari hiyo kwa kutumia maneno yako mwenyewe kwa njia rahisi na iliyo wazi.
Kumbuka: Shiriki na wengine mambo uliyojifunza ili kuwatia moyo, na si ili kujionyesha.—1 Kor. 8:1.