Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • yb90 kur. 253-255
  • Kuzaa Tunda Kwa Uvumilivu

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Kuzaa Tunda Kwa Uvumilivu
  • 1990 Kitabu cha Mwaka cha Mashahidi wa Yehova
  • Habari Zinazolingana
  • Shikamana na Tengenezo la Yehova
    Tengenezo Linalofanya Mapenzi ya Yehova
  • ‘Wenye Furaha Ni Wale Ambao Wamevumilia’
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1990
  • Fuliza Kuzaa Matunda Kwa Uvumilivu
    Huduma Yetu ya Ufalme—1990
  • Uvumilivu Unaopata Ushindi
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1991
Pata Habari Zaidi
1990 Kitabu cha Mwaka cha Mashahidi wa Yehova
yb90 kur. 253-255

Kuzaa Tunda Kwa Uvumilivu

Ulimwengu huu unatoa habari njema chache sana, ikiwa unatoa zozote. Hata hivyo Yehova amekusudia kwamba wakati huu habari njema kuhusu matukio yenye kupendeza ulimwengu wote mzima lazima zijulishwe. Kulingana na Ufunuo 14:6, habari njema za milele zapaswa kuendea “kila taifa na kabila na ulimi na kikundi cha watu.” Akiwa ndiye mwenye daraka sana kuhusu yaliyomo katika habari njema hizi, Yehova anafanya sehemu yake. Tunajua kwamba Kristo Yesu na malaika watakatifu wanafanya sehemu yao. Kama ilivyoonyeshwa katika ripoti hii ya ulimwenguni pote, sisi tulio hapa duniani, tukiwa washiriki wa ama mabaki watiwa-mafuta au mkutano mkubwa, tunafanya sehemu yetu katika kueneza habari njema hizi, ambazo zinatia ndani agizo linalokaziwa katika andiko letu la mwaka wa 1989, “Ogopeni Mungu na kumpa yeye utukufu.”—Ufu. 14:7, NW.

Maandishi yanaonyesha vizuri kwamba, pote katika tufe, sisi, tukiwa Mashahidi wa Yehova, tunafanya hivyo tukiwa na umoja, na kama tokeo la baraka ya Mungu, jitihada zetu zinazaa tunda. Ni pendeleo lisilo na kifani kumtukuza Mungu kwa utendaji wetu wa kiroho wenye kuzaa tunda. Hatupaswi kulichukua vivi hivi tu, kwa kuwa ni lazima mtu athibitishwe na Mungu kuwa anafaa kukabidhiwa habari njema. (1 The. 2:4) Kwenye 2 Wakorintho 2:14-17 mtume Paulo anatukumbusha pia kwamba tumepelekwa na Mungu kwa kuandamana na Kristo ili tutoe maarifa yenye kutoa uhai katika kila mahali. Kudumisha ufaaji wetu wa kiroho kwa ajili ya utumishi wa Mungu ili tuwe tunastahili vya kutosha kwa ajili ya pendeleo hili kunaleta manufaa nyingi.

Kila mwaka makumi ya maelfu wanabatizwa watu wa namna zote wanapokuja kwenye maarifa yaliyo sahihi ya ukweli. (1 Tim. 2:4) Mwaka huu uliopita tu, 263,855 walibatizwa kwa kuonyesha wakfu wao. Hii iliweka daraka kubwa zaidi juu ya kila mmoja atunze kondoo hawa. Zaidi ya hilo, makundi mengi, au vitovu vya ibada iliyotakata, vilianzishwa. Sasa kuna makundi 60,192 ya Mashahidi wa Yehova ulimwenguni pote. Haya ni 2,522 zaidi ya mwaka uliotangulia.

Sasa mamilioni wanatambua kwamba manufaa za kweli zinapatikana, si kwa kupata kile ambacho ulimwengu unatoa, bali kwa kuwa na uhusiano wa karibu pamoja na Yehova, wakiwa wanafunzi wa Yesu Kristo. (Mt. 16:26) Kwa kutii na kuhofu Mungu, tunajinufaisha wenyewe, tukipata burudisho kwa nafsi zetu. (Isa. 48:17, 18; Mt. 11:28-30) Kuwa wahudumu wa habari njema wenye kuzaa matunda ni jambo lenye kupendeza sana. Hakika amri za Mungu si mzigo.—1 Yoh. 5:3.

Hata hivyo, ulimwengu mwovu ukiwa chini ya uvutano wa Ibilisi unasababisha matatizo mengi. Yesu alionya kwamba ingekuwa hivyo. (Yoh. 16:33) Kwa sababu hiyo, kueneza ukweli si jambo rahisi sikuzote. Kweli za Biblia hazipendwi na wale ambao hawana hofu ya kimungu. Kama ilivyotabiriwa, “nyakati za hatari” zipo hapa. (2 Tim. 3:1, 12, 13) Hii inasaidia kueleza kwa nini sisi sote tunapata mitihani na majaribu ya aina moja au nyingine.

Mwaka huu uliopita upinzani wa waziwazi uliwaka moto katika Burundi na Rwanda, kama ulivyowaka moto wakati uliopita katika sehemu nyingine katika Afrika. Katika sehemu nyingine, akina ndugu walitupwa gerezani na kutaabishwa. Katika mabara 36, ijapokuwa marufuku walieneza habari njema, nazo zilizaa tunda. Na namna gani wale wanaoishi katika nyumba zilizogawanyika? Wengi wanatendwa vibaya au kudhihakiwa na washiriki wa jamaa wenye kupinga au wenzi wa ndoa wasioamini. Katika nchi zenye utajiri mwingi, akina ndugu wanakuwa chini ya mikazo yenye hila kutoka kwa vitu vilivyomo ulimwenguni na kutoka mavutano ya kufuatia vitu vya kimwili. (1 Yoh. 2:15-17) Yote haya yametaka uvumilivu.

Kwa kuwa Mashahidi wa Yehova wanavumilia na kutumikia, hata chini ya hali ngumu, kazi inasonga mbele. Kwa wazi ripoti hii inathibitisha kwamba hatuchoki, hata tupatwe na majaribu gani! Kwa kweli tunashukuru kuwa miongoni mwa wale ambao, “baada ya kulisikia lile neno wakiwa na moyo mzuri na mwema, wanalishika na kuzaa tunda kwa uvumilivu”!—Luka 8:15, NW.

Unaweza kufikiria ndugu wangapi ambao wamevumilia kwa uaminifu katika kumtumikia Mungu? Kwa njia halisi kuna maelfu yao. Hawajakosa thawabu ambazo Yehova ameahidi. (Ebr. 6:10-12) Hakika Yehova atawakumbuka, kwa kuwa wanataka kuvumilia katika kazi iliyo njema. (Rum. 2:6, 7) Kielelezo chao chema ni kitia-moyo kwetu. Sisi pia na tuendelee kuvumilia jaribu, tukijua kwamba Yehova ameahidi kuwapa taji ya uhai wale wanaoendelea kumpenda yeye. (Yak. 1:12) Lakini hata kabla ya kupata zawadi hiyo, lo, ni baraka nyingi kama nini ambazo tunamiminiwa sasa! Ile sifa ya kimungu ya uvumilivu inatuwezesha tutimize huduma yetu siku baada ya siku na mwaka baada ya mwaka. Hakuna kitu kinachoweza kulinganishwa na furaha yetu ya kufanya penzi la Mungu sasa na kuwa na tumaini hakika la wakati ujao ulio mwangavu. Ndivyo alivyohisi mtume Paulo kuhusu jambo hilo, na kwa sababu hiyo yeye aliwatia moyo Wakristo wasichoke kutenda yaliyo mema.—Gal. 6:9.

Ndugu zetu waliohudhuria mikusanyiko katika Polandi Agosti ya mwaka wa utumishi uliopita walipata baraka zisizoweza kupimika. (Mal. 3:10) Kwa miaka mingi, maelfu katika Ulaya ya Mashariki walikuwa hawajapata fursa ya kuhudhuria mikusanyiko katika mabara yao wenyewe. Je! wamevunjika moyo kwa kuwa hawajaweza kuwa na manufaa kama zile zinazoonewa shangwe na akina ndugu walio katika hali zenye kupendeleka zaidi? Sivyo hata kidogo! Kwa kweli, Yehova aliwatimizia mambo fulani ingawa hawakuwa na mapendeleo fulani ambayo wengine walizoelea kupata kwa ukawaida. Ni mambo gani ambayo yametimizwa upande wao? Paulo alieleza jambo hilo vizuri wakati alipoandika: “Na tufurahi katika dhiki pia; tukijua ya kuwa dhiki, kazi yake ni kuleta saburi; na kazi ya saburi ni uthabiti wa moyo; na kazi ya uthabiti wa moyo ni tumaini; na tumaini halitahayarishi.” (Rum. 5:3-5) Ndiyo, tokeo la uvumilivu wao ni upendeleo wa kimungu na utimizo wa tumaini lao wanapoendelea kuwa wahudumu wenye kutenda na wenye kuzaa tunda.—2 Pet. 1:5-8.

Kwa kweli, tuna kila sababu ya kushangilia, ndiyo, kuchachawa katika yale ambayo Yehova amefanya na anafanyia watu wake. Kama ilivyoonyeshwa kwa nguvu nyingi kwenye “Ujitoaji Kimungu” Mikusanyiko ya Wilaya, umoja na upatano wa watu wa Yehova unaonyesha kwamba wana roho yake. Mabaki watiwa-mafuta wamo katika muungamano pamoja na Kristo Yesu, mzabibu wa kweli. Mkutano mkubwa wenye kuongezeka leo ukiwa unaunga mkono, sisi sote tunaweza hivyo kuzaa matunda mengi chini ya mpango wa Mkulima Mkuu, Yehova. Na tukae karibu na Yehova na Mwana wake, kwa kuwa hatuwezi kufanya lolote tukiwa mbali nao.—Yoh. 15:1-5.

Tutumikiapo pamoja wakati wa mwaka huu mpya wa utumishi, hakika Yehova atatusaidia tuendelee kuzaa tunda kwa uvumilivu. Na tuwe “wenye moyo mkuu na kusema: ‘Yehova ndiye msaidiaji wangu.’”—Ebr. 13:6.

Ndugu zenu,

BARAZA LINALOONGOZA LA MASHAHIDI WA YEHOVA

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki