Kuhubiri na Kufundisha Duniani Kote—2008 Jumla Kuu
KILA mwaka tunasoma katika kitabu hiki jinsi ndugu wanavyojitahidi kuwasaidia watu wamjue na kumpenda Yehova Mungu. Kazi hiyo ya kuwasaidia watu imefanywa kwa kiwango kisicho na kifani. Hakuna tengenezo ambalo lingeweza kulipa mamilioni ya watu kutangaza ujumbe wowote kwa watu wa mataifa mengi hivyo. Lakini katika kazi yao ya kuwafundisha watu Biblia, Mashahidi wa Yehova hawatafuti kufaidika kifedha. Wanafuata maagizo ambayo Yesu aliwapa wanafunzi wake miaka elfu mbili hivi iliyopita: “Mlipokea bure, toeni bure.” (Mt. 10:8) Unapotafakari mambo ambayo yametimizwa katika mwaka wa utumishi uliopita, tua ufikirie yale ambayo yamefanywa na wale wanaojitolea kwa kupenda na bila ubinafsi, kwa sababu wamechochewa na upendo wa Mungu.
2008 Jumla Kuu
Ofisi za Tawi za Mashahidi wa Yehova: 115
Idadi ya Nchi Zinazoripoti: 236
Idadi ya Makutaniko: 103,267
Waliohudhuria Ukumbusho Ulimwenguni Pote: 17,790,631
Waliokula Mkate na Kunywa Divai Ulimwenguni Pote: 9,986
Kilele cha Wahubiri wa Ufalme: 7,124,443
Wastani wa Wahubiri Watendaji Kila Mwezi: 6,829,455
Asilimia ya Ongezeko Kupita 2007: 2.1
Idadi ya Waliobatizwa: 289,678
Wastani wa Mapainia Wasaidizi Kila Mwezi: 321,986
Wastani wa Mapainia Kila Mwezi: 732,912
Jumla ya Saa Zilizotumiwa Shambani: 1,488,658,249
Wastani wa Mafunzo ya Biblia Kila Mwezi: 7,133,760
Katika mwaka wa utumishi wa 2008, Mashahidi wa Yehova walitumia zaidi ya dola milioni 141 za Marekani kwa ajili ya mapainia wa pekee, wamishonari, na waangalizi wanaosafiri katika kazi yao ya kuhubiri.
◼ Ulimwenguni pote kuna wahudumu 19,820 waliowekwa rasmi kufanya kazi katika ofisi za tawi. Wote hao ni sehemu ya Kikundi cha Ulimwenguni Pote cha Watumishi wa Pekee wa Wakati Wote cha Mashahidi wa Yehova.
[Chati katika ukurasa wa 32-39]
RIPOTI YA MWAKA WA UTUMISHI WA 2008 YA MASHAHIDI WA YEHOVA ULIMWENGUNI POTE
(Ona nakala iliyochapishwa)
[Ramani katika ukurasa wa 40-42]
(Ona nakala iliyochapishwa)