Kuhubiri na Kufundisha Ulimwenguni Pote—Jumla Kuu 2007
RIPOTI ifuatayo ya mwaka wa utumishi uliopita inasisimua kama nini! Huu si mkusanyo wa habari tu. Badala yake, kurasa zifuatazo zinaonyesha upendo mkubwa na ujitoaji wa wanaume, wanawake, na watoto wanaomhofu Mungu ulimwenguni pote. Naam, ripoti hii inatuonyesha jinsi ndugu na dada wamejidhabihu, na inaonyesha jitihada na mali zilizotumiwa kuhubiri habari njema “mpaka sehemu ya mbali zaidi ya dunia.” (Mdo. 1:8) Dhabihu hizo, ziwe kubwa ama ndogo, zinathaminiwa sana na Yehova Mungu na Mwana wake, Yesu Kristo. (Zab. 50:14; Luka 21:1-4) Pia, ripoti ya mwaka inatukumbusha kwamba kazi ya kuokoa uhai inaweza tu kufanywa kwa “nguvu ambazo Mungu hutoa.” (1 Pet. 4:11) Kwa hiyo, unapotafakari kuhusu ripoti ya mwaka na mambo yaliyoonwa yafuatayo, na ‘uendelee kujipatia nguvu katika Bwana na katika uwezo wa nguvu zake.’—Efe. 6:10.
Jumla Kuu 2007
Ofisi za Tawi za Mashahidi wa Yehova: 113
Idadi ya Nchi Zinazoripoti: 236
Idadi ya Makutaniko: 101,376
Waliohudhuria Ukumbusho Ulimwenguni Pote: 17,672,443
Waliokula Mkate na Kunywa Divai Ulimwenguni Pote: 9,105
Kilele cha Wahubiri wa Ufalme: 6,957,854
Wastani wa Wahubiri Watendaji Kila Mwezi: 6,691,790
Asilimia ya Ongezeko Kupita 2006: 3.1
Idadi ya Waliobatizwa: 298,304
Wastani wa Mapainia Wasaidizi Kila Mwezi: 312,741
Wastani wa Mapainia Kila Mwezi: 678,638
Jumla ya Saa Zilizotumiwa Shambani: 1,431,761,554
Wastani wa Mafunzo ya Biblia Kila Mwezi: 6,561,426
Katika mwaka wa utumishi wa 2007, Mashahidi wa Yehova walitumia zaidi ya dola milioni 121 za Marekani kwa ajili ya mapainia wa pekee, wamishonari, na waangalizi wanaosafiri katika kazi yao ya kuhubiri.
◼ Ulimwenguni pote kuna wahudumu 19,581 waliowekwa rasmi kufanya kazi katika ofisi za tawi. Wote hao ni sehemu ya Kikundi cha Watumishi wa Pekee wa Wakati Wote wa Mashahidi wa Yehova.
[Chati katika ukurasa wa 32-39]
RIPOTI YA MWAKA WA UTUMISHI WA 2007 YA MASHAHIDI WA YEHOVA ULIMWENGUNI POTE
(Ona nakala iliyochapishwa)
[Ramani katika ukurasa wa 40-42]
(Ona nakala iliyochapishwa)