Kuhubiri na Kufundisha Duniani Kote—Jumla Kuu za 2009
YEHOVA anawapa watu wote zawadi yenye thamani. Zawadi hiyo ni habari njema ya Ufalme. Sisi ambao tumepokea zawadi hiyo na tunampenda Yehova, tuna pendeleo la kuwasaidia wengine pia waipate. Kufanya hivyo hutupa shangwe kwa kuwa tunajua kwamba tunamfurahisha Yehova na pia wale wanaoipokea. Kwa kweli tunapohubiri habari njema tunaonyesha kwamba tunampenda Mungu na majirani. (Mt. 22:37-40) Katika kurasa zinazofuata, utaona jinsi ambavyo watu wa Yehova wanaonyesha upendo huo kwa kuhubiri ulimwenguni pote.
Jumla Kuu za 2009
Ofisi za Tawi za Mashahidi wa Yehova: 118
Idadi ya Nchi Zinazoripoti: 236
Idadi ya Makutaniko: 105,298
Waliohudhuria Ukumbusho Ulimwenguni Pote: 18,168,323
Waliokula Mkate na Kunywa Divai Ulimwenguni Pote: 10,857
Kilele cha Wahubiri wa Ufalme: 7,313,173
Wastani wa Wahubiri Watendaji Kila Mwezi: 7,046,419
Asilimia ya Ongezeko Kupita 2008: 3.2
Idadi ya Waliobatizwa: 276,233
Wastani wa Mapainia Wasaidizi Kila Mwezi: 304,551
Wastani wa Mapainia Kila Mwezi: 794,317
Jumla ya Saa Zilizotumiwa Shambani: 1,557,788,344
Wastani wa Mafunzo ya Biblia Kila Mwezi: 7,619,270
Katika mwaka wa utumishi wa 2009, Mashahidi wa Yehova walitumia zaidi ya dola milioni 140 za Marekani kwa ajili ya mapainia wa pekee, wamishonari, na waangalizi wanaosafiri katika kazi yao ya kuhubiri.
◼ Ulimwenguni pote kuna wahudumu 19,829 waliowekwa rasmi kufanya kazi katika ofisi za tawi. Wote hao ni sehemu ya Kikundi cha Ulimwenguni Pote cha Watumishi wa Pekee wa Wakati Wote cha Mashahidi wa Yehova.
[Chati katika ukurasa wa 32-39]
RIPOTI YA MWAKA WA UTUMISHI WA 2009 YA MASHAHIDI WA YEHOVA ULIMWENGUNI POTE
(Ona nakala iliyochapishwa)
[Ramani katika ukurasa wa 40-42]
(Ona nakala iliyochapishwa)