Utendaji wa Mashahidi wa Yehova Katika Nyakati za Kisasa
Norway
Wazia kuhubiri habari njema katika nchi ya mikono-bahari, milima, barafu, theluji, na mbawala—nchi ambayo mianga ya kaskazini yenye kumeremeta huonekana angani wakati wa majira ya baridi kali. Hivyo ndivyo nchi ya Norway ilivyo. Soma kuwahusu ndugu waliosafiri kwa mashua na viatu vya kuteleza kwenye theluji ili kuwafikia watu wanaoishi maeneo ya mbali, na pia ndugu aliyetembea kwenda mikutanoni bila viatu. Soma pia kuhusu jinsi Wakristo walivyoonyesha imani na ujasiri chini ya utawala wenye kukandamiza wa Wanazi.
Rwanda
Upendo wa kujidhabihu ambao Yesu alisema ungewatambulisha wanafunzi wake unaonekana wazi katika historia ya nchi hii ya Afrika. Licha ya chuki ya kikabila iliyosababisha mauaji ya jamii nzima-nzima, watu wa Yehova walihatarisha uhai wao na hata nyakati nyingine wakaupoteza ili kuwasaidia wenzao. Hili ni simulizi lisilosahaulika kuhusu uvumilivu chini ya mnyanyaso na marufuku, na utimilifu licha ya kukabili mambo magumu, majaribu, na matukio yenye kuogopesha sana.