Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • yb14 uku. 99
  • “Utakufa Kabla ya Mwaka Huu Kwisha”

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • “Utakufa Kabla ya Mwaka Huu Kwisha”
  • 2014 Kitabu cha Mwaka cha Mashahidi wa Yehovah
  • Habari Zinazolingana
  • Ninaipenda Sana Nchi ya Sierra Leone
    2014 Kitabu cha Mwaka cha Mashahidi wa Yehovah
  • Kazi ya Kufanya Wanafunzi Imefinyanga Maisha Yangu
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2007
  • Nimeazimia Kumtumikia Yehova
    2014 Kitabu cha Mwaka cha Mashahidi wa Yehovah
  • Kwa Nini Uhudhurie Mikutano Kwenye Jumba la Ufalme?
    Vijana Huuliza
Pata Habari Zaidi
2014 Kitabu cha Mwaka cha Mashahidi wa Yehovah
yb14 uku. 99

SIERRA LEONE NA GUINEA

“Utakufa Kabla ya Mwaka Huu Kwisha”

Zachaeus Martyn

  • ALIZALIWA 1880

  • ALIBATIZWA 1942

  • MAELEZO MAFUPI KUMHUSU Alianza upainia alipokuwa na umri wa miaka 72.

Picha katika ukurasa wa 99

ZACHAEUS hakufundishwa Biblia na mtu yeyote. Hata hivyo, baada ya kusoma kitabu Salvation na The Harp of God, akajua kwamba ameipata kweli.

Jumapili moja, mwaka 1941, Zachaeus alitoka asubuhi na mapema ili kwenda kuhudhuria mkutano wa Mashahidi kwa mara ya kwanza, ambao ulikuwa ukifanyika katika eneo lenye mteremko mkali umbali wa kilometa nane kutoka mahali alipoishi. Bila kujua mkutano ungeanza saa ngapi, aliwasili saa kadhaa mapema. Zachaeus alikaa na kungojea akina ndugu wawasili. Baada ya kuhudhuria mikutano kwa Jumapili tatu katika Jumba la Ufalme, akaliambia Kanisa la Anglikana lililokuwa katika eneo lao waondoe jina lake kwenye vitabu vyao.

Rafiki yake wa karibu, ambaye alikuwa mshiriki wa kanisa hilo, alimdhihaki akisema, “Mzee, ikiwa utaendelea kutembea hizo kilometa nane ukipanda na kushuka mlima huu kwenda kwenye jumba la watu hao, utakufa kabla ya mwaka huu kwisha.” Kwa miaka mitano aliendelea kumwona Zachaeus akipanda na kushuka mlima ule mara mbili kwa wiki. Kisha yule rafiki akafa ghafla! Miaka ishirini na tano baadaye, bado Zachaeus alikuwa mwenye nguvu.

Zachaeus aliendelea kumtumikia Yehova kwa uaminifu hadi alipokufa akiwa na umri wa miaka 97.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki