Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • yb17 kur. 130-131
  • Mmekuwa Wapi Siku Hizo Zote?

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Mmekuwa Wapi Siku Hizo Zote?
  • 2017 Kitabu cha Mwaka cha Mashahidi wa Yehova
  • Habari Zinazolingana
  • Makasisi Wenye Hasira Watendewa kwa Upole
    Masimulizi ya Mashahidi wa Yehova
  • Mwalimu Abadili Maoni Yake
    Amkeni!—2009
  • Maandishi ya Kale Yenye Thamani
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2013
  • Niliona kwa Macho Yangu Mwenyewe Kile Ambacho Biblia Inasema!
    2017 Kitabu cha Mwaka cha Mashahidi wa Yehova
Pata Habari Zaidi
2017 Kitabu cha Mwaka cha Mashahidi wa Yehova
yb17 kur. 130-131

GEORGIA

Mmekuwa Wapi Siku Hizo Zote?

Artur Gerekhelia

  • ALIZALIWA 1956

  • ALIBATIZWA 1991

  • HISTORIA FUPI Miezi minane tu baada ya kubatizwa, aliacha nyumba pamoja na biashara yake iliyokuwa imesitawi, ili aende kutumikia eneo lenye uhitaji mkubwa.

Artur Gerekhelia

MUDA mfupi tu ulikuwa umepita tangu nibatizwe wazee waliponiuliza ikiwa ningependa kupanua utumishi wangu. Katika Mei 4, 1992, nilihudhuria mkutano uliokuwa umetayarishwa kwa ajili ya wale waliotaka kuhamia maeneo yenye uhitaji mkubwa. Siku iliyofuata, mimi na mwandamani wangu wa utumishi tulihamia kwenye bandari ya Batumi, eneo la Ajaria.

Nilikuwa na wasiwasi sana siku ya kwanza kuhubiri katika eneo hilo. Nilijiuliza hivi: ‘Nitaanzishaje mazungumzo na watu?’ Nilishangazwa na itikio la mwanamke wa kwanza tuliyekutana naye, ambaye alisema hivi kwa msisimko, “Mmekuwa Wapi Siku Hizo Zote?” Hamu yake ya kuwajua vizuri Mashahidi ilikuwa kubwa sana hivi kwamba tulianza kujifunza naye Biblia siku iliyofuata!

Kabla ya kwenda Batumi, tulipokea orodha ya anwani za watu wanaopendezwa. Kwa kuwa tulikuwa wageni katika jiji hilo, tuliomba watu watuelekeze. Wengi hawakuweza kutusaidia kwa sababu muda mrefu haukuwa umepita tangu majina ya mitaa mingi kubadilishwa, lakini walipendezwa na ujumbe wetu. Muda si muda, tulikuwa tukijifunza na vikundi vya watu 10 hadi 15.

Miezi minne tu baada ya kuwasili, idadi ya waliokuwa wakihudhuria mikutano kwa ukawaida ilikuwa watu zaidi ya 40. Kwa hiyo tukajiuliza hivi: ‘Ni nani atakayewatunza watu hawa wapya?’ Kisha, kwa sababu ya vurugu jijini Abkhazia kati ya jeshi la Georgia na waasi, washiriki wote wa kutaniko nililoshirikiana nalo mwanzoni wakahamia Batumi. Kutaniko jipya lenye wazee na mapainia wazoefu likaanzishwa kwa siku moja!

Kikundi kikijifunza Biblia
    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki