Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • ijwex makala 30
  • Walithamini Barua Zake

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Walithamini Barua Zake
  • Masimulizi ya Mashahidi wa Yehova
  • Habari Zinazolingana
  • Machozi Yake Yafutwa na Mungu
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2001
  • Vipi Ikiwa Sipendi Shule?
    Vijana Huuliza
  • Matokeo Aliyopata Yalimshangaza
    Masimulizi ya Mashahidi wa Yehova
  • Waliendelea Kuhubiri Licha ya Janga
    Masimulizi ya Mashahidi wa Yehova
Pata Habari Zaidi
Masimulizi ya Mashahidi wa Yehova
ijwex makala 30
Mwanamume apokea barua iliyoandikwa kwa mikono.

Walithamini Barua Zake

Brooke ni Shahidi wa Yehova na anaishi Marekani. Katika kipindi cha COVID-19 alihubiri kwa kuandika barua. Brooke aliandika barua nyingi kila juma. Hata hivyo, baada ya mwaka mmoja na nusu alikata tamaa. Kufikia wakati huo, ni mtu mmoja tu aliyekuwa amejibu barua zake na mtu huyo alimwonya Brooke asijaribu kumwandikia tena. Brooke alihisi jitihada zake zinaambulia patupu.

Hata hivyo, baada ya muda, dada anayeitwa Kim alimwambia Brooke kwamba alikuwa amezungumza na mteja fulani kwenye benki anayofanya kazi. Mteja huyo alimwambia Kim kwamba alikuwa amepata barua iliyoandikwa kwa mkono kutoka kwa Shahidi wa Yehova. Kumbe barua hiyo ilikuwa imeandikwa na Brooke! Mteja huyo alirudi benki juma linalofuata. Katika mazungumzo yao alimwambia Kim kwamba angependa kuhudhuria mikutano yetu. Kipindi hicho tulikuwa tukifanya mikutano kupitia mtandao.

Baada ya muda, Shahidi mwingine anayeitwa David, alimwambia Brooke kwamba mfanyakazi mwenzake alikuwa amepokea barua kutoka kwa Brooke. Mfanyakazi huyo aliguswa moyo sana alipoona kwamba barua hiyo ilikuwa imeandikwa kwa mkono. Alimwambia David: “Laiti watu wengi zaidi wangewajali wenzao kiasi hiki.” David alitumia fursa hiyo kumweleza mwanamume huyo habari zaidi kuhusu Biblia na akaahidi kumletea machapisho. Mwanamume huyo alisikiliza na akasema kwamba anatazamia kwa hamu kupata machapisho.

Ukweli ni kwamba, huenda Mashahidi wa Yehova wasijue mbegu wanayopanda katika huduma inapochipuka. (Mhubiri 11:5, 6) Hata hivyo, mambo hayo yaliyoonwa yalimsaidia Brooke kuona fungu muhimu analotimiza katika kazi ya kuhubiri.​—1 Wakorintho 3:6.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki