Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w01 8/1 uku. 18
  • Machozi Yake Yafutwa na Mungu

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Machozi Yake Yafutwa na Mungu
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2001
  • Habari Zinazolingana
  • Endelea Kuwa na Nguvu Kiroho Unapomtunza Mshiriki wa Familia Aliye Mgonjwa
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2010
  • Kwa Nini Baba Alikufa?
    Amkeni!—1994
  • Walithamini Barua Zake
    Masimulizi ya Mashahidi wa Yehova
  • Namna Gani Nikishikwa na Mahaba kwa Mtu Asiye Mwamini?
    Amkeni!—1994
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2001
w01 8/1 uku. 18

Ripoti ya Watangazaji wa Ufalme

Machozi Yake Yafutwa na Mungu

WATU wanaoishi kupatana na sheria na kanuni za Yehova hubarikiwa sana. Ingawa si rahisi sikuzote kufanya mabadiliko yanayohitajika, wanaweza kupata msaada na kitia-moyo kwa urahisi. (Zaburi 84:11) Jambo hili lililoonwa huko Kusini-Mashariki ya Asia linadhihirisha hilo.

Alipokuwa likizoni, Shahidi mmoja wa Ufaransa alizungumza na mwenye duka fulani aitwaye Kima kuhusu kusudi la Yehova kwa dunia. Pia alimwachia Kim kitabu Unaweza Kuishi Milele Katika Paradiso Duniani. Alipokuwa akitazama-tazama kitabu hicho, Kim aliona maneno, “atafuta kabisa kila chozi kutoka katika macho yao.” (Ufunuo 21:4) “Andiko hilo lilinigusa moyo sana,” akumbuka Kim. “Kwa kuwa nilionekana kuwa mtu mwenye furaha nilipofanya kazi dukani, hakuna yeyote ambaye angedhani kwamba nilipofika nyumbani jioni, nilikuwa nikilia hadi nilipopatwa na usingizi.” Akieleza sababu iliyomfanya ahuzunike, Kim asema hivi: “Nilikuwa nimeishi na mwanamume fulani kwa miaka 18 na sikuwa na furaha hata kidogo kwa sababu alikataa tuhalalishe ndoa. Nilitaka kumwacha, lakini sikuwa na ujasiri wa kufanya hivyo kwa kuwa nilikuwa nimeishi naye kwa muda mrefu sana.”

Muda mfupi baadaye, Kim alikubali kujifunza Biblia na Shahidi mmoja wa Yehova aitwaye Linh. “Nilitaka sana kutenda kupatana na mafundisho ya Biblia,” asema Kim. “Kwa mfano, niliacha kuabudu wazazi wangu wa kale, ingawa watu wa familia yangu walinipinga sana. Isitoshe, nilijaribu kuhalalisha ndoa na yule mwanamume niliyeishi naye lakini akakataa. Wakati huo mgumu, yule Shahidi kutoka Ufaransa aliendelea kunitumia vichapo vya Biblia, naye Linh akanitia moyo sana. Subira na utegemezo wa dada hawa wawili ulinisaidia kuvumilia mpaka nikamjua vizuri mwanamume niliyekuwa nikiishi naye. Niligundua kwamba alikuwa na ‘wake’ 5 na watoto 25! Jambo hilo lilinipa ujasiri wa kumwacha.

“Haikuwa rahisi kuacha nyumba kubwa nzuri na kwenda kuishi katika nyumba ndogo. Isitoshe, mwanamume huyo alijaribu kunilazimisha kwenda kuishi naye tena na hata akatisha kuniharibia sura kwa kunimwagia asidi nikikataa. Kwa msaada wa Yehova, niliweza kufanya yaliyo sawa.” Kim alizidi kufanya maendeleo na hatimaye akabatizwa Aprili 1998. Isitoshe, dada zake wawili na mwanaye ambaye ni tineja, walianza kujifunza Biblia pamoja na Mashahidi wa Yehova.

“Nilikuwa nikifikiri kwamba sikuzote maisha yangu yangekuwa bila tumaini,” asema Kim. “Hata hivyo, leo mimi nina furaha, na silii tena usiku. Yehova amefuta machozi kutoka katika macho yangu.”

[Maelezo ya Chini]

a Majina yamebadilishwa.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki