Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • ijwyp makala 7
  • Vipi Ikiwa Sipendi Shule?

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Vipi Ikiwa Sipendi Shule?
  • Vijana Huuliza
  • Habari Zinazolingana
  • Je, Niache Shule?
    Amkeni!—2010
  • Sababu Gani Ujifunze Shuleni?
    Kupata Faida Zote za Ujana Wako
  • Niache Shule?
    Maswali Ambayo Vijana Huuliza—Majibu Yafanyayo Kazi, Buku la 1
  • Ukurasa wa Pili
    Amkeni!—2012
Pata Habari Zaidi
Vijana Huuliza
ijwyp makala 7
Tineja aliyevunjika moyo akiwa amesimama mbele ya makabati ya shule.

VIJANA HUULIZA

Vipi Ikiwa Sipendi Shule?

Walimu ni wakali. Kushinikizwa na marafiki. Mitihani yenye kuchosha akili, na rundo la masomo ya shule ya kufanyiwa nyumbani. Huenda una sababu nzuri unaposema hupendi shule.a Tineja anayeitwa Rachelb anasema hivi:

“Laiti ningeweza kuwa mahali pengine popote isipokuwa shuleni. Laiti ningeweza kuwa ufuoni mwa bahari au pamoja na rafiki zangu au hata ningekuwa nikiwasaidia wazazi wangu kupika au kufanya usafi!”

Ikiwa unahisi kama Rachel, basi unahisi kana kwamba uko jela na unalazimika kungoja mpaka kifungo chako kiishe wakati unapohitimu shule. Je, unaweza kuuona wakati unaotumia shuleni kwa njia bora zaidi?

Je, wajua? Unapositawisha maoni yanayofaa kuhusu shule, unaweza kudhibiti hisia zako na kuacha kuiona kama mahali pa kuvumiliwa tu. Shule inaweza kukupatia fursa ya kukuza stadi utakazohitaji ukiwa mtu mzima.

Ili kuwa na mtazamo mzuri kuhusu shule, jaribu kukazia fikira mambo yafuatayo:

Alama inayoonyesha kitabu na kalamu.

Elimu yako. Kadiri unavyojifunza, ndivyo kadiri utakavyoweza kutatua matatizo yako ya wakati ujao kazini na katika sehemu nyingine za maisha yako badala ya kuwategemea wengine sikuzote. Jiulize, ‘Hata kama kuna mambo ambayo sipendi shuleni, ni manufaa gani ninayopata kutokana na elimu yangu?’

Kanuni ya Biblia: “Ilinde hekima inayotumika na uwezo wa kufikiri.”​—Methali 3:21.

Ili kupata habari zaidi, ona makala yenye kichwa “Nifanye Nini Ikiwa Ninaanguka Mitihani?”

Alama inayoonyesha orodha.

Tabia zako. Tabia nzuri unazojifunza shuleni zinaweza kukufundisha kusimamia vizuri wakati wako, kuwa mwenye kuwajibika, na kuwa mfanyakazi mwenye bidii—hizo ni sifa utakazohitaji utakapokuwa mtu mzima. Jiulize: ‘Ni katika njia gani kwamba tabia nzuri ninazojifunza shuleni zinanisaidia kuwa mtu mwenye kuwajibika na mfanyakazi mzuri? Ninaweza kuboreshaje tabia hizo?’

Kanuni ya Biblia: “Kila aina ya kazi ngumu ina faida.”​—Methali 14:23.

Ili kupata habari zaidi, ona makala yenye kichwa “Ninaweza Kutumiaje Vizuri Muda Wangu?”

Alama inayoonyesha watu wawili wakiwa na mazungumzo.

Uhusiano wako na wengine. Kuchangamana na wanafunzi wenzako kunaweza kukusaidia uwe mwenye huruma na uwaheshimu wengine. Kijana anayeitwa Joshua anasema, “kujifunza kuwasiliana na watu ni muhimu kama vile tu kujifunza historia na sayansi. Ni ustadi utakaoutumia katika maisha yako yote.” Jiulize, ‘Nimejifunza masomo gani shuleni kuhusu kuishi vizuri na wengine—hata wale ambao malezi yao au dini yao ni tofauti na yangu?’

Kanuni ya Biblia: “Fuatilieni amani pamoja na watu wote.”​—Waebrania 12:14.

Ili kupata habari zaidi, ona makala yenye kichwa “Ninaweza Kuboreshaje Ustadi Wangu wa Kuzungumza?”

Alama inayoonyesha mtu akitembea barabarani.

Wakati wako ujao. Shule inaweza kukusaidia utambue mambo unayoweza kufanya vizuri na uweke malengo kulingana nayo. Msichana anayeitwa Brooke anasema hivi: “Hata huenda ukapata ustadi fulani hususa, kama nilivyopata mimi. Ujuzi huo utakusaidia kupata kazi unapohitimu.” Jiulize: ‘Nitajitegemezaje baada ya kuhitimu? Ninaweza kuhakikishaje kwamba ninajifunza yale yatakayonisaidia kupata kazi hiyo?’

Kanuni ya Biblia: “Fikiria njia utakayochukua.”​—Methali 4:26, Biblia Habari Njema.

a Kanuni nyingi zinazozungumziwa kwenye makala hii pia zitawasaidia vijana wanaosomea nyumbani.

b Baadhi ya majina yamebadilishwa.

Vijana wenzako wanasema nini

  • Madison.

    “Ilinibidi nishirikiane na watu tofauti-tofauti katika vikundi vya kufanya utafiti. Kwa kufanya hivyo, nilijifunza kusikiliza watu ambao malezi yao na namna ya maisha yao yalikuwa tofauti na yangu. Wanafunzi wenzangu walikuwa wazuri na waliniheshimu kwa sababu walijua mimi ni mwenye fadhili na sikuwachambua-chambua.”​—Madison.

  • Ryan.

    “Nilijifunza jinsi ya kuwa na mtazamo unaofaa kuhusu wanafunzi wenzangu. Wengi wao walikuwa wakijaribu kuwa watu wazuri. Kwa hiyo nilitafuta fursa ya kuwaambia jambo lenye kutia moyo kutoka katika Biblia.”​—Ryan.

  • Brooke.

    “Shule hukusaidia uwe na ustadi wa kushirikiana na wengine. Kwa kuwa unashinda siku nzima pamoja na wanafunzi wenzako, unajifunza kile unachoweza kusema na kile ambacho hupaswi kusema, jinsi ya kuwa mwenye subira, na jinsi ya kushiriki vitu na wengine. Katika somo la michezo, unashiriki na wengine katika vikundi, na hilo linakufundisha jinsi ya kufanya mambo kwa pamoja—jambo ambalo huwezi kujifunza ukiwa peke yako.”​—Brooke.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki