Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • ijwhf makala 35
  • Jinsi ya Kuepuka “Talaka ya Uzeeni”

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Jinsi ya Kuepuka “Talaka ya Uzeeni”
  • Msaada kwa Ajili ya Familia
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • Ni nini ambacho husababisha talaka ya uzeeni?
  • Kile unachoweza kufanya
  • Je, Kupatana Kwawezekana?
    Amkeni!—1999
  • Kuchagua Talaka
    Amkeni!—1999
  • Urafiki Unapokuwa wa Karibu Kupita Kiasi
    Amkeni!—2013
  • Nyumba Iliyogawanyika—Jinsi Talaka Inavyowaathiri Vijana
    Amkeni!—2009
Pata Habari Zaidi
Msaada kwa Ajili ya Familia
ijwhf makala 35
Wenzi wa ndoa wenye umri mkubwa ambao hawana furaha, kila mmoja akiwa mbali na mwenzake. Kila mmoja akiangalia kando.

MSAADA KWA AJILI YA FAMILIA | NDOA

Jinsi ya Kuepuka “Talaka ya Uzeeni”

Kati ya mwaka wa 1990 na 2015, idadi ya talaka kati ya watu wenye umri wa miaka 50 au zaidi iliongezeka maradufu nchini Marekani, na idadi ya talaka kati ya watu walio na umri wa zaidi ya miaka 65 iliongezeka mara tatu. Ni nini kinachosababisha talaka za uzeeni? Unaweza kuilindaje ndoa yako isiathiriwe?

Katika makala hii

  • Ni nini ambacho husababisha talaka ya uzeeni?

  • Unaweza kufanya nini?

  • Mwongozo wa mazungumzo

Ni nini ambacho husababisha talaka ya uzeeni?

  • Mara nyingi, uhusiano wa wenzi wa ndoa wenye umri mkubwa ulianza mapema sana kudhoofika hatua kwa hatua. Baada ya muda, wanaanza kusitawisha mapendezi tofauti kisha wanakosa kufurahia mambo pamoja. Au baada ya watoto wao kuwa watu wazima na kuondoka nyumbani, wenzi hao wanatambua kwamba wamekuwa wakizingatia zaidi majukumu yao ya kuwa wazazi kwa muda mrefu sana hivi kwamba wamesahau jinsi ya kuwa mume na mke.

  • Katika miaka ya karibuni, watu wanaodai kuwa wataalamu wamekuwa wakiwashauri wenzi wa ndoa watangulize hisia zao binafsi kwa kujiuliza: ‘Je, ndoa yangu inanifurahisha?’ ‘Je, inanifanya niwe mtu mzuri zaidi?’ ‘Je, mwenzi wangu wa ndoa anatosheleza mahitaji yangu ya kihisia?’ Ikiwa hafanyi hivyo, wataalamu hao wanasema, jitangulize wewe na hisia zako, yaani, mtaliki mwenzi wako na uanze maisha yako upya.

  • Watu hawaioni talaka kuwa jambo baya tena. Mwanasosholojia Eric Klinenberg aliandika hivi: “Miaka ya nyuma, ikiwa mtu hakufurahishwa na mwenzi wake wa ndoa na alitaka talaka, ilibidi atoe sababu nzuri za kuchukua hatua hiyo. Lakini leo ni kinyume kabisa: Ikiwa huridhishwi na ndoa yako, unapaswa kutoa sababu nzuri kwa nini unaendelea kukaa katika ndoa hiyo, kwa sababu leo watu wanaamini jambo muhimu zaidi ni kufanya kinachokufaa wewe.”a

Ukweli ni kwamba talaka sio mwisho wa matatizo, badala yake ni mwanzo wa matatizo mengine mapya. Kwa mfano, uchunguzi mmoja ulionyesha kwamba “talaka ya uzeeni huvuruga mtu kiuchumi, hasa wanawake.”

Kuna jambo lingine la kufikiria. Kitabu Don’t Divorce kinasema hivi: “Hata ukijaribu kubadili maisha yako, wewe bado ni mtu yuleyule. Umefanya nini kubadili njia yako ya kuwasiliana na wengine, kwa kuwa ni wazi hukufaulu kuwasiliana na mwenzi wako wa ndoa? Umefanya nini ili kubadili jinsi unavyoshughulikia hali ya kutoelewana?”b

Kile unachoweza kufanya

  • Kubali mabadiliko. Hakuna uhusiano ambao hubaki vilevile sikuzote. Huenda uhusiano wako na mwenzi wako umebadilika kwa sababu watoto wenu waliondoka au kwa sababu mapendezi yenu nyote wawili yamebadilika. Badala ya kung’ang’ania mambo yalivyokuwa zamani, jaribu kuboresha mambo yalivyo sasa.

    Wenzi wa ndoa wenye umri mkubwa wameketi mezani. Mke anatazama picha za familia akiwa na mwana wao huku mume wake akitazama kiti kitupu akiwa mezani.

    Kanuni ya Biblia: “Usiulize: ‘Mbona siku za zamani zilikuwa bora kuliko hizi?’ kwa maana hukuuliza hivyo kwa hekima.”​—Mhubiri. 7:10.

  • Jengeni urafiki wa karibu. Je, unaweza kuonyesha upendezi katika mapendezi ya sasa ya mwenzi wako, au je, unaweza kumwalika mwenzi wako ashiriki katika jambo unalopenda kwa sasa? Je, mnaweza kuwa na jambo moja mnalopendezwa nalo sasa ambalo mnaweza kulifurahia kwa pamoja? Lengo lenu linapaswa kuwa kutumia wakati pamoja, ili wewe na mwenzi wako mhisi mko katika ndoa badala ya kuhisi kama watu wanaotumia chumba kimoja tu.

    Wenzi wa ndoa wakipalilia bustani yao pamoja wakiwa na furaha.

    Kanuni ya Biblia: “Kila mmoja na aendelee kutafuta, si faida yake mwenyewe, bali faida ya yule mtu mwingine.”​—1 Wakorintho 10:24.

  • Muwe na zoea la kuzungumza kwa njia nzuri. Usimpuuze mwenzi wako eti kwa sababu mmeishi pamoja kwa muda mrefu. Ongea kwa heshima, na ujitahidi kuonyesha adabu uliyoonyesha mlipokuwa mnachumbiana. Tumia maneno kama “tafadhali” na “asante.” Mwonyeshe mwenzi wako upendo, na umwambie unathamini mambo anayokufanyia.

    Mwanamume mzee akishikilia mwavuli huku akimfungulia mke wake mlango wa gari.

    Kanuni ya Biblia: “Mtendeane kwa fadhili, huruma nyororo.”​—Waefeso 4:32.

  • Kumbukeni pindi nzuri mlizokuwa nazo. Tazameni picha zenu za harusi pamoja, au mwangalie picha za matukio mengine mliyofurahia pamoja. Kufanya hivyo kunaweza kuwasaidia kudumisha au kurudisha tena upendo na heshima katika ndoa yenu.

    Wenzi wa ndoa wenye furaha wakitazama picha pamoja.

    Kanuni ya Biblia: “Kila mtu kati yenu anapaswa kumpenda mke wake kama anavyojipenda mwenyewe; kwa upande mwingine, mke anapaswa kumheshimu sana mume wake.”​—Waefeso 5:33.

a Kutoka kitabu Going Solo—The Extraordinary Rise and Surprising Appeal of Living Alone

b Msingi pekee wa Kimaandiko wa talaka ni uasherati. (Mathayo 19:5, 6, 9) Tazama makala “Je, Biblia Inaruhusu Talaka?”

Mwongozo wa mazungumzo

Kwanza, kila mmoja anaweza kufikiria maswali yafuatayo. Kisha mzungumzie majibu pamoja.

  • Ni sifa zipi za mwenzi wako zilizokuvutia awali?

  • Baada ya muda kupita, umetambua mabadiliko gani katika uhusiano wenu?

  • Ungependa kuona marekebisho gani katika ndoa yenu?

  • Unaweza kujengaje urafiki wa karibu na mwenzi wako?

  • Mwenzi wako anaweza kufanya nini ili kuimarisha urafiki wenu?

  • Ungependa mwenzi wako aseme au kufanya mambo gani madogo-madogo yenye fadhili na heshima?

  • Wewe na mwenzi wako mnaweza kufurahia mambo gani pamoja?

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki