Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • ijwyp makala 100
  • Vipi Ikiwa Nimevunja Sheria Fulani ya Nyumbani?

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Vipi Ikiwa Nimevunja Sheria Fulani ya Nyumbani?
  • Vijana Huuliza
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • Mambo ambayo hupaswi kufanya
  • Njia bora zaidi ya kushughulikia tatizo
  • Ninaweza Kufanya Nini Ili Wazazi Wangu Waniamini?
    Vijana Huuliza
  • Kwa Nini Wazazi Wangu Hawaniachi Nifurahie Maisha?
    Vijana Huuliza
  • Kwa Nini Kuna Sheria Nyingi Sana?
    Maswali Ambayo Vijana Huuliza—Majibu Yafanyayo Kazi, Buku la 2
  • Kwa Nini Wazazi Wangu Hawaniamini?
    Amkeni!—2008
Pata Habari Zaidi
Vijana Huuliza
ijwyp makala 100
Wazazi wakiwa na wasiwasi, wanazungumza na binti yao baada ya binti huyo kuchelewa kurudi nyumbani.

VIJANA HUULIZA

Vipi Ikiwa Nimevunja Sheria Fulani ya Nyumbani?

Karibu familia zote zina sheria—sheria zinazohusu mambo kama vile muda wa kurudi nyumbani, matumizi ya teknolojia, na jinsi ya kujiendesha na kuwatendea wengine.

Vipi ikiwa utavunja sheria fulani? Huwezi kubadilisha jambo hilo, lakini unaweza kuzuia hali isiwe mbaya zaidi. Makala hii itakusaidia kufanya hivyo.

  • Mambo ambayo hupaswi kufanya

  • Njia bora zaidi ya kushughulikia tatizo

  • Vijana wenzako wanasema nini?

Mambo ambayo hupaswi kufanya

  • Ikiwa wazazi wako hawajui kama umevunja sheria fulani, unaweza kushawishika kuficha jambo hilo.

  • Ikiwa wanajua kwamba umevunja sheria, unaweza kushawishika kutafuta visingizio au kumlaumu mtu mwingine.

Hizo si njia bora za kushughulikia tatizo. Kwa nini? Kwa sababu kujaribu kuficha kosa lako au kutafuta visingizio visivyo na msingi ni ishara ya kwamba bado wewe ni mtoto. Ni kana kwamba unawaambia wazazi wako bado unahitaji kukua zaidi.

“Kusema uwongo hakukusaidii. Baada ya muda, ukweli utajulikana na adhabu utakayopewa itakuwa kali zaidi kuliko ungesema kosa lako mapema.”—Diana

Njia bora zaidi ya kushughulikia tatizo

  • Kubali kosa lako. Biblia inasema: “Anayefunika makosa yake hatafanikiwa.” (Methali 28:13) Wazazi wako wanajua kwamba huwezi kuwa mkamilifu. Lakini swali ni, Unaweza kuwa mnyoofu?

    “Wazazi wako watakuonea huruma ikiwa utasema kweli. Ukisema kweli, watakuamini zaidi kwa unyoofu wako.”—Olivia

  • Omba msamaha. Biblia inasema: “Mjivike unyenyekevu.” (1 Petro 5:5, Maelezo ya chini.) Unahitaji kuwa mnyenyekevu ili uweze kusema “Nisamehe”na kujizuia kuanza kuorodhesha visingizio.

    “Watu ambao hutoa visingizio mara kwa mara hudhoofisha dhamiri yao. Hatimaye, hata wakifanya jambo baya hawatajisikia vibaya tena.”—Heather

  • Kubali matokeo ya kosa lako. Biblia inasema: “Sikilizeni nidhamu.” (Methali 8:33) Epuka kunung’unika, na ukubali adhabu yoyote ambayo utapewa na wazazi wako.

    “Kadiri unavyozidi kunung’unika unapopewa adhabu, ndivyo unavyofanya hali yako iwe mbaya zaidi. Jaribu kukubaliana na vizuizi ulivyowekewa, na usikazie fikira mambo ambayo huwezi kufanya kwa wakati huo.”—Jason

  • Jitahidi kufanya wazazi wako waanze kukuamini tena. Biblia inasema: ‘Vua utu wa zamani unaopatana na mwenendo wenu wa zamani.’ (Waefeso 4:22) Anza kufanya mambo ambayo yanaonyesha kwamba unaweza kuaminika tena.

    “Ukiwa na kawaida ya kufanya maamuzi kwa hekima na kuwaonyesha wazazi wako kwamba hutarudia makosa uliyofanya, hatimaye watakuamini tena.”—Karen

DOKEZO: Ili kuonyesha kwamba unaweza kuaminika tena, fanya zaidi ya kile ambacho wazazi wako wamekwambia ufanye. Kwa mfano, unapoenda mahali fulani, wataarifu unapokuwa njiani ukirudi—hata ikiwa hutachelewa. Ni kana kwamba unawaambia, ‘Ninataka mniamini tena.’

Vijana wenzako wanasema nini?

Darius.

“Kuwaficha wazazi wako jambo ulilofanya, ni sawa na kudanganya. Mwisho wa siku, jambo hilo litajulikana, na likijulikana, hali haitakuwa nzuri kwako. Ni bora ungesema ukweli toka mwanzoni.”—Darius

Sierra.

“Unapomlaumu mtu mwingine kwa jambo ambalo wewe umefanya, unaonekana wewe bado ni mtoto na kwamba hujakomaa vya kutosha kuwajibika kwa makosa yako. Wazazi wako wataacha kukuamini ikiwa hutawajibika vya kutosha kuomba msamaha.”—Sierra

Pitio: Vipi Ikiwa Nimevunja Sheria Fulani ya Nyumbani?

  • Kubali kosa lako. Wazazi wako wanajua kwamba huwezi kuwa mkamilifu. Lakini swali ni, Unaweza kuwa mnyoofu?

  • Omba msamaha. Sema, “Nisamehe,” kutoka moyoni, na ujizuie kuanza kuorodhesha visingizio.

  • Kubali matokeo ya kosa lako. Kubaliana na adhabu yoyote ambayo utapewa na wazazi wako.

  • Jitahidi kufanya wazazi wako waanze kukuamini tena. Anza kufanya mambo ambayo yanaonyesha kwamba unaweza kuaminika tena.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki