Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • mrt makala 16
  • Msaada kwa Wanaotendewa kwa Jeuri Nyumbani

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Msaada kwa Wanaotendewa kwa Jeuri Nyumbani
  • Habari Zaidi
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • Si kosa lako hivi kwamba unatendewa kijeuri
  • Unaweza kupata msaada
  • Hauko peke yako
  • Kutendewa kwa jeuri kutakwisha
  • Mwisho wa Jeuri ya Nyumbani
    Amkeni!—1993
  • Ni Nini Husababisha Jeuri ya Nyumbani?
    Amkeni!—1993
  • Jeuri Iathiripo Nyumbani
    Amkeni!—1993
  • Unaweza Kushinda Matatizo Yanayoidhuru Familia
    Siri ya Furaha ya Familia
Pata Habari Zaidi
Habari Zaidi
mrt makala 16
Mwanamke akitazama machweo ya jua kuelekea baharini akiwa na tumaini.

Msaada kwa Wanaotendewa kwa Jeuri Nyumbani

“Jeuri dhidi ya wanawake ni tatizo kubwa la kiafya linalohitaji kushughulikiwa haraka kama tu ugonjwa wa mlipuko,” linasema Shirika la Afya Duniani. Shirika hilo linakadiria kwamba asilimia 30 ya “wanawake wote walioolewa au waliokuwa katika mahusiano, wametendewa kwa jeuri iwe kwa kupigwa kihalisi au kutendewa vibaya kingono” na wenzi wao. Ripoti ya Umoja wa Mataifa inakadiria kwamba katika kipindi cha mwaka mmoja, wanawake 137 walikufa kila siku duniani baada ya kutendewa kwa jeuri na mwenzi wao au mtu wa familia.a

Ijapokuwa takwimu hizo zinaonyesha ukubwa wa tatizo la kutendewa kwa jeuri nyumbani, haziwezi kutuelezea maumivu halisi na ya kihisia wanayopata wale wanaotendewa kwa jeuri.

Je, unatendewa kwa jeuri? Au je, unamfahamu mtu anayetendewa hivyo? Ikiwa ndiyo, ona msaada unaopatikana katika Biblia.

Si kosa lako hivi kwamba unatendewa kijeuri

Unaweza kupata msaada

Hauko peke yako

Kutendewa kwa jeuri kutakwisha

Jinsi unavyoweza kumsaidia anayetendewa kwa jeuri

Si kosa lako hivi kwamba unatendewa kijeuri

Biblia inasema nini: “Kila mmoja wetu atatoa hesabu kwa Mungu kwa ajili yake mwenyewe.”—Waroma 14:12.

Kumbuka jambo hili: Anayekutendea kwa jeuri atatoa hesabu.

Ikiwa mwenzi wako anakulaumu wewe kwamba matendo yako ndiyo chanzo cha yeye kukutendea kwa jeuri, hayuko sahihi. Wake wanapaswa kupendwa wala si kutendewa kwa jeuri.—Wakolosai 3:19.

Wakati mwingine, huenda anayekutendea kwa jeuri anafanya hivyo kwa sababu ya matatizo ya kihisia, malezi, au matumizi mabaya ya kileo. Hata hivyo, bado atatoa hesabu machoni pa Mungu kwa jinsi anavyokutendea. Pia, ni jukumu lake kufanya yote awezayo kubadili tabia yake.

Unaweza kupata msaada

Biblia inasema nini: “Mambo hufanikiwa kupitia washauri wengi.”—Methali 15:22.

Kumbuka jambo hili: Ikiwa unahisi hauko salama au haujui la kufanya, wengine wanaweza kukusaidia.

Kwa nini huenda ukahitaji msaada kutoka kwa wengine? Kuna mambo mengi yanayohusika mtu anapotendewa kwa jeuri. Huenda isiwe rahisi kwako kuamua jambo linalofaa kufanya kwa kuwa haujui ni mambo gani muhimu kati ya haya:

  • Usalama wako

  • Uamuzi utakaowafaa watoto wako

  • Hali yako ya kifedha

  • Upendo wako kwa mwenzi wako

  • Tamaa yako ya kuendelea na uhusiano ikiwa mwenzi wako ataacha vitendo vyake

Ni kweli kwamba huenda ukahisi umechanganyikiwa na usijue jambo la kufanya. Unaweza kupata wapi msaada?

Rafiki au ndugu wa familia anayetegemeka anaweza kukusaidia kwa maneno na matendo. Kuongea na mtu anayekujali kunaweza kuwa na matokeo mazuri sana.

Piga simu katika vituo vinavyotoa msaada kwa wanaotendewa kwa jeuri ambapo utapata msaada bila kukawia. Wahudumu wa vituo hivyo wanaweza kukusaidia kujua jambo la kufanya ili uwe salama. Ikiwa mwenzi wako atatambua kwamba ana tatizo na kwa unyoofu atataka kubadilika, wahudumu wa vituo hivyo wanaweza kumsaidia kwa kumwambia hatua za kwanza anazopaswa kuchukua.

Vyanzo vingine vya msaada wakati wa dharura vinaweza kukusaidia ukiwa hatarini na unahitaji msaada wa haraka. Vyanzo hivyo vinatia ndani madaktari, wauguzi, au wataalamu wengine waliozoezwa kushughulikia hali hizo.

Hauko peke yako

Biblia inasema nini: “Yehovab yuko karibu na wale waliovunjika moyo; huwaokoa waliopondeka roho.”—Zaburi 34:18.

Kumbuka jambo hili: Mungu ameahidi kukusaidia.

Yehova anakujali sana. (1 Petro 5:7) Anaelewa vizuri sana mawazo na hisia zako za ndani kabisa. Anaweza kukufariji kupitia Neno Lake, Biblia. Angependa uzungumze naye kupitia sala. Unaposali, unaweza kumwomba akupatie hekima na nguvu utakazohitaji ili kushughulikia hali yako.—Isaya 41:10.

Kutendewa kwa jeuri kutakwisha

Biblia inasema nini: “Wataketi, kila mtu chini ya mzabibu wake na chini ya mtini wake, na hakuna yeyote atakayewaogopesha.”—Mika 4:4, maelezo ya chini.

Kumbuka jambo hili: Biblia inaahidi kwamba hivi karibuni familia zote zitaishi kwa amani.

Ni Yehova Mungu peke yake atakayeondoa kabisa matatizo yetu yote. Biblia inatuahidi hivi: “Naye atafuta kila chozi kutoka katika macho yao, na kifo hakitakuwapo tena, wala maombolezo wala kilio wala maumivu hayatakuwapo tena.” (Ufunuo 21:4) Wakati huo hatutakumbuka tena mambo mabaya badala yake tutafurahia mambo mengi mazuri. (Isaya 65:17) Biblia inakupatia wewe ahadi hizo za wakati ujao utakaokuwa na amani.

a Ingawa makala hii inataja wanawake kuwa ndio wanaotendewa kwa jeuri, mambo mengi yanayotajwa yanawahusu pia wanaume wanaokabili hali hizo.

b Yehova ni jina la Mungu kama linavyoonyeshwa katika Biblia.

Jinsi unavyoweza kumsaidia anayetendewa kwa jeuri

Je, unamfahamu mtu anayetendewa kwa jeuri? Hata kama wewe si mtaalamu aliyezoezwa, bado unaweza kutoa msaada.c

Sikiliza ukionyesha hisia-mwenzi. (Yakobo 1:19) Mwambie kwamba uko tayari kumsikiliza, lakini usimlazimishe kuongea. Mhakikishie kwamba unaamini mambo anayosema.​—Methali 20:5.

Chapisho moja lililozungumzia kutendewa kwa jeuri lilisema hivi: “Inahitaji ujasiri kwa mtu kuzungumza nawe. Mara nyingi watu wanaotendewa kwa jeuri huficha au huhisi kuwa ni jambo la kawaida kutendewa hivyo. Kwa kawaida, masimulizi yao ni ya kweli. Huenda ikawa vigumu kwako kuamini kwamba mtu fulani unayemfahamu vizuri anaweza kumtendea kwa jeuri mwenzi wake. Hata hivyo, mtu anayefanya vitendo hivyo vya jeuri huenda akatenda kana kwamba hana hatia anapokuwa nawe.”

Mtie moyo. (1 Wathesalonike 5:11) Zungumza naye katika njia itakayomfanya ahisi kwamba anathaminiwa. Mwambie kwamba unamjali. Mkumbushe sifa zake nzuri. Na mtie moyo atafute msaada.

Msaidie. (Methali 17:17) Mpe msaada hususa kama vile kuwaangalia watoto wake kwa muda fulani mfupi au kwa kumpikia chakula. Zungumza naye na uhakikishe kwamba ana mpango hususa wa kuwa salama, kama vile mahali atakapoenda iwapo atapatwa na hali ya dharura.

Mhakikishie kwamba anaweza kufanya maamuzi yake mwenyewe. (Wagalatia 6:5) Mpatie taarifa na zungumzieni mambo ya kufanya. Hata hivyo, usimfanyie uamuzi.

c Ikiwa anayetendewa kwa jeuri ni mwanamke na wewe unayetaka kutoa msaada ni mwanamume, unaweza kufanya hivyo kwa kiwango fulani na wakati uleule ukimtia moyo atafute msaada kutoka kwa rafiki yake wa karibu na anayetegemeka ambaye ni mwanamke.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki