Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • mrt makala 29
  • Jinsi ya Kudhibiti Wasiwasi

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Jinsi ya Kudhibiti Wasiwasi
  • Habari Zaidi
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • Madokezo ya jinsi ya kudhibiti wasiwasi
  • Ninawezaje Kuacha Kuwa na Wasiwasi Mwingi Mno?
    Amkeni!—2001
  • Usihangaike
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Toleo la Watu wote)—2016
  • Mathayo 6:34—“Msihangaike Kamwe Kuhusu Kesho”
    Mistari ya Biblia Yafafanuliwa
  • 2 Hutusaidia Kutatua Matatizo
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Toleo la Watu wote)—2018
Pata Habari Zaidi
Habari Zaidi
mrt makala 29
Mwanamume mzee akiwa na wasiwasi.

Jinsi ya Kudhibiti Wasiwasi

Kuwa na wasiwasi kupita kiasi kunaweza kuathiri mwili na hisia zako. Hata kunaweza kukusababishia matatizo makubwa zaidi ya tatizo ambalo awali lilifanya uwe na wasiwasi.

Madokezo ya jinsi ya kudhibiti wasiwasi

  • Nyuso yenye wasiwasi.

    Punguza kiasi cha habari mbaya unazopata. Si lazima upate taarifa kuhusu kila tatizo linaloendelea ulimwenguni. Kufuatilia kupita kiasi taarifa mbaya kutakuongezea hofu na kukuvunja moyo.

    Kanuni ya Biblia: “Roho iliyopondeka humfyonza mtu nguvu.”—Methali 17:22.

    “Ni rahisi sana kuzoea kupata habari mpya na zenye kushtua, lakini hilo si jambo zuri. Wasiwasi wangu hupungua sana ninapopunguza kiasi cha habari ninazopata.”—John.

    Jambo la kufikiria: Ni mara ngapi ambazo kwa kweli unahitaji kupata habari za karibuni zaidi?

  • Saa.

    Uwe na ratiba na uifuate. Amka mapema, kula chakula, fanya kazi za nyumbani, na lala wakati uleule kwa kufuata ratiba yako. Kuwa na ratiba kutakusaidia uhisi kwamba mambo hayajabadilika maishani mwako, na hilo litakupunguzia wasiwasi.

    Kanuni ya Biblia: “Mipango ya wenye bidii hakika huleta mafanikio.”—Methali 21:5.

    “Ugonjwa wa COVID-19 ulipoanza, niliacha kabisa kufuata ratiba yangu, nilitumia wakati mwingi kutazama burudani. Nilitaka kutumia vizuri wakati wangu, hivyo nilipanga ratiba ya mambo ninayopaswa kufanya kila siku.”—Joseph.

    Jambo la kufikiria: Je, una ratiba inayokusaidia uhisi kwamba umetimiza jambo fulani kila siku?

  • Nyuso yenye furaha.

    Kazia fikira mambo mazuri. Kukazia fikira hali mbaya na ambazo huwezi kubadili kutakufanya uzidi kuwa na wasiwasi. Badala yake, fikiria mambo mawili au matatu yanayofanya uwe mwenye shukrani.

    Kanuni ya Biblia: “Mjionyeshe kuwa wenye shukrani.”—Wakolosai 3:15.

    “Kusoma Biblia hunisaidia kuepuka kutafuta habari mbaya na badala yake kukazia fikira mambo mazuri. Huenda hilo likaonekana kuwa jambo rahisi sana, lakini ni jambo la uhakika!”—Lisa.

    Jambo la kufikiria: Je, wewe hukazia fikira mambo mabaya unayokabili maishani na kusahau mambo mema?

  • Zawadi.

    Wafikirie wengine. Badala ya kujitenga—jambo ambalo ni rahisi kufanya hasa ukiwa na wasiwasi—fikiria namna unavyoweza kuwasaidia walio na uhitaji.

    Kanuni ya Biblia: “Mkiangalia, si faida zenu wenyewe, bali pia faida za wengine.”—Wafilipi 2:4.

    “Kuwasaidia wengine huniletea furaha. Ninafanya mambo ambayo yatawafanya wahisi vizuri, na wakati uleule, ninapunguza wasiwasi wangu. Kwa kweli, ninakosa muda wa kuwa na wasiwasi.”—Maria.

    Jambo la kufikiria: Kati ya watu unaowajua, ni nani walio na uhitaji wa pekee, na unaweza kuwasaidiaje?

  • Moyo.

    Tunza afya yako. Fanya mazoezi na pumzika vya kutosha. Kula vyakula vyenye afya. Kutunza afya yako kunaweza kuboresha mtazamo wako kuhusu maisha na kukusaidia kuondoa wasiwasi wowote ulio nao.

    Kanuni ya Biblia: “Mazoezi ya kimwili ni yenye faida.”—1 Timotheo 4:8, maelezo ya chini.

    “Mimi na mwana wangu hatuwezi kufanya mazoezi nje kama tunavyopenda, hivyo tuna ratiba ya kufanya mazoezi ndani ya nyumba. Kufanya hivyo kumetusaidia tuhisi vizuri na kutendeana kwa fadhili.”—Catherine.

    Jambo la kufikiria: Je, unahitaji kuboresha mlo wako na kufanya mazoezi zaidi ili uwe na afya njema?

Mbali na kutumia madokezo hayo ili kupunguza wasiwasi, watu wengi wamenufaika na kujifunza kuhusu tumaini hakika la wakati ujao linalopatikana katika Biblia. Ona makala “Ufalme wa Mungu Utatimiza Nini?”

Mistari ya Biblia kuhusu wasiwasi

Zaburi 55:22: “Mtupie Yehova mzigo wako, naye atakutegemeza.”a

Maana yake: Tunaweza kutupa mzigo wetu unaotia ndani mambo yanayofanya tuwe na wasiwasi, kwa kusali kwa Mungu. Sala ni mawasiliano halisi na Muumba, anayetutunza na ambaye “hutufariji katika majaribu yetu yote.”—2 Wakorintho 1:3, 4.

Methali 12:25, maelezo ya chini: “Mahangaiko yaliyo moyoni mwa mtu huulemea moyo, lakini neno jema huuchangamsha.”

Maana yake: Wasiliana na watu wa familia au marafiki wanaoweza kukutia moyo na kukuambia mambo ya kufanya ili kuboresha hali yako.

Mathayo 6:27: “Ni nani kati yenu ambaye kwa kuhangaika anaweza kurefusha uhai wake kwa mkono mmoja?”

Maana yake: Mara nyingi kuwa na wasiwasi hakuleti manufaa yoyote. Hakuboreshi hali yako au kukupatia suluhisho la tatizo lako.

Mathayo 6:31, 32: “Kwa hiyo msihangaike kamwe na kusema, ‘Tutakula nini?’ au, ‘Tutakunywa nini?’ au, ‘Tutavaa nini?’ . . . Baba yenu wa mbinguni anajua kwamba mnahitaji vitu hivi vyote.”

Maana yake: Yehova Mungu anajua tunapohitaji chakula, mavazi na malazi hata kabla ya sisi kufahamu.

a Yehova ni jina la kibinafsi la Mungu.—Zaburi 83:18

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki