Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • mrt makala 59
  • Wakristo na Vita—Biblia Inasema Nini?

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Wakristo na Vita—Biblia Inasema Nini?
  • Habari Zaidi
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • Kile ambacho Biblia inasema hasa
  • Wakristo na vita leo
  • Dini na Vita Nchini Ukrainia—Biblia Inasema Nini?
    Habari Zaidi
  • 2022: Mwaka Uliojaa Misukosuko—Biblia Inasema Nini?
    Habari Zaidi
  • Urusi Yashambulia Ukrainia
    Habari Zaidi
  • Vita Nchini Ukrainia Vyaingia Mwaka wa Pili—Biblia Inatoa Tumaini Gani?
    Habari Zaidi
Pata Habari Zaidi
Habari Zaidi
mrt makala 59
Kasisi akibariki ndege ya kivita, akiinyunyizia maji matakatifu.

YURI LASHOV/AFP via Getty Images

ENDELEA KUKESHA!

Wakristo na Vita—Biblia Inasema Nini?

Kama ambavyo tumeona wakati wa vita nchini Ukrainia, viongozi wengi Wakristo wanawatia watu moyo waunge mkono upande fulani katika vita hivyo. Ona jinsi viongozi wa dini wameunga mkono pande zote:

  • “Ni heshima na shukrani kubwa kwa mashujaa wote wanaotetea nchi yao ya Ukrainia kutokana na mkandamizaji . . . Sikuzote mioyo yetu, sala zetu, na utegemezo wetu upo pamoja nanyi.”​—Askofu Epiphanius wa Kwanza wa Kyiv, kama ilivyoripotiwa katika The Jerusalem Post, la Machi 16, 2022.

  • “Mkuu wa Kanisa Othodoksi la Urusi aliongoza ibada ya pekee kwa ajili ya wanajeshi wa Urusi Jumapili na kuwatia moyo wailinde nchi yao ‘kama Warusi tu wanavyoweza’ huku Moscow ikiendeleza kampeni yake nchini Ukrainia.​—Shirika la Habari la Reuters, Aprili 3, 2022.

Je, Wakristo wanapaswa kushiriki katika vita? Biblia inasema nini?

Kile ambacho Biblia inasema hasa

Biblia inaonyesha kwamba wale ambao ni wafuasi wa kweli wa Yesu Kristo hawajihusishi katika vita.

  • “Rudisha upanga wako mahali pake, kwa maana wote wanaochukua upanga wataangamia kwa upanga.”​—Mathayo 26:52.

    Je, kweli mtu anayeunga mkono vita au anayepigana katika vita anatii maneno ya Yesu?

  • “Ninawapa ninyi amri mpya, kwamba mpendane; kama vile ambavyo nimewapenda, nanyi mpendane vivyo hivyo. Kwa jambo hili wote watajua kwamba ninyi ni wanafunzi wangu—mkiwa na upendo miongoni mwenu.”​—Yohana 13:34, 35.

    Je, mtu anayeunga mkono upande fulani katika vita anaonyesha upendo ambao Yesu alisema ungewatambulisha wanafunzi, au wafuasi wake?

Ili upate habari zaidi, soma makala yenye kichwa “Je, Ukristo Unaunga Mkono Vita?”

Wakristo na vita leo

Je, inapatana na akili kuwatazamia Wakristo kutojihusisha katika vita leo? Ndiyo. Biblia ilitabiri kwamba katika siku zetu, kipindi kinachoitwa “siku za mwisho,” kungekuwa na watu kutoka katika mataifa yote ambao kupatana na mafundisho ya Yesu, “hawatajifunza vita tena kamwe.”​—Isaya 2:2, 4.

  • Ili ujifunze mengi zaidi, soma mfululizo wa makala wenye kichwa “Mungu Ana Maoni Gani Kuhusu Vita?” katika gazeti Mnara wa Mlinzi.

Hivi karibuni Yehova,a yule “Mungu wa amani,” atatumia serikali yake ya mbinguni kuwakomboa watu “kutoka katika ukandamizaji na ukatili.”​—Wafilipi 4:9; Zaburi 72:14.

  • Ili uone jinsi hilo litakavyotimia, tazama video Ufalme wa Mungu Ni Nini?

Tunakualika kwa uchangamfu kutazama kusanyiko letu la 2022 lenye kichwa “Fuatilia Amani!” Programu hiyo inaweza kukusaidia kupata amani ya moyoni licha ya matukio mabaya yanayowafanya watu wengi kulemewa na mahangaiko. Pakua programu hiyo au uitazame kwenye mtandao. Huhitaji kujisajili.

a Yehova ni jina la kibinafsi la Mungu.​—Zaburi 83:18.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki