Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • mrt makala 72
  • Je, Bado Ukweli Ni Muhimu?

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Je, Bado Ukweli Ni Muhimu?
  • Habari Zaidi
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • Je, ukweli unaweza kupatikana leo?
  • Unaweza kupataje kweli?
  • Uwongo ulianzia wapi?
  • Kwa nini uwongo ni jambo la kawaida leo?
  • Kwa nini kweli ni muhimu?
  • Kwa nini Mungu anataka mimi nijue kweli?
  • Je, Mungu atakomesha uwongo?
  • Kumwiga Mungu wa Ukweli
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2003
  • Wakristo Huabudu kwa Roho na Kweli
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2002
  • Kwa Nini Utafute Kweli?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1995
  • Usiache Ukweli Ukuponyoke
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1986
Pata Habari Zaidi
Habari Zaidi
mrt makala 72
Mwanasiasa akiuchochea umati mkubwa kwenye mkutano wa kisiasa.

Je, Bado Ukweli Ni Muhimu?

Je, unahisi kwamba siku hizi si rahisi kutambua kati ya ukweli na uwongo? Ni kana kwamba siku hizi watu wanafanya maamuzi wakiongozwa na hisia na maoni ya kibinafsi na si kwa kutegemea ukweli au mambo ya hakika. Ulimwenguni pote leo, watu wengi hawaamini ukweli unaweza kupatikana popote.

Mtazamo huo ulikuwepo tangu zamani. Miaka 2,000 hivi iliyopita, Gavana Mroma Pontio Pilato alimwuliza Yesu hivi kwa kejeli: “Kweli ni nini?” (Yohana 18:38) Ingawa Pilato hakusubiri Yesu ajibu, swali lake lilikuwa muhimu. Biblia inatusaidia tupate jibu lenye kuridhisha, na inaweza kutupatia mwongozo katika ulimwengu huu ambao watu wanashindwa kutofautisha kati ya ukweli na uwongo.

Je, ukweli unaweza kupatikana leo?

Ndiyo. Biblia inatumia neno “kweli” inaporejelea mambo ya hakika na pia kuhusu mambo ambayo ni sahihi na yanayofaa. Inafundisha kwamba Yehovaa Mungu ndiye Chanzo cha ukweli kamili, hata inasema kwamba yeye ni “Mungu wa ukweli.” (Zaburi 31:5) Biblia ina kweli kutoka kwa Mungu, na inalinganisha kweli hiyo na mwangaza, kwa sababu kweli inaweza kutuongoza katika ulimwengu huu ambao hauna mwelekeo.​—Zaburi 43:3; Yohana 17:17.

Unaweza kupataje kweli?

Mungu hataki tukubali kweli iliyo katika Biblia bila kuichunguza. Badala yake, anatualika tuichanganue kwa kutumia nguvu zetu za kufikiri na si kwa kutegemea hisia zetu. (Waroma 12:1) Anataka tumjue na kumpenda ‘kwa akili yetu yote,’ naye anatutia moyo tujihakikishie ikiwa mambo tunayojifunza katika Biblia ni ya kweli.​—Mathayo 22:37, 38; Matendo 17:11.

Uwongo ulianzia wapi?

Biblia inasema kwamba uwongo ulianzishwa na adui ya Mungu, Shetani Ibilisi, ambaye Biblia inamwita “baba ya uwongo.” (Yohana 8:44) Aliwaambia wanadamu wa kwanza uwongo kumhusu Mungu. (Mwanzo 3:1-6, 13, 17-19; 5:5) Tangu wakati huo, Shetani ameendelea kueneza uwongo na kuficha ukweli kumhusu Mungu.​—Ufunuo 12:9.

Kwa nini uwongo ni jambo la kawaida leo?

Biblia inaziita siku zetu kuwa “siku za mwisho.” Leo, Shetani anazidi kuwapotosha watu. Ni jambo la kawaida kwa watu kuwaambia wengine uwongo ili kuwalaghai. (2 Timotheo 3:1, 13) Pia, uwongo unatawala katika dini nyingi leo. Kama Biblia ilivyotabiri kuhusu siku zetu, watu ‘wanajikusanyia walimu ili masikio yao yafurahishwe,’ wakichagua ‘kuacha kuisikiliza ile kweli.’​—2 Timotheo 4:3, 4.

Kiongozi wa dini akiwa ameshika Biblia huku akizungumza na umati unaompigia makofi.

Kwa nini kweli ni muhimu?

Ukweli ndio msingi wa kuwafanya watu waaminiane. Watu wanapokosa kuaminiana, urafiki na jamii kwa ujumla hudhoofika. Biblia inasema kwamba Mungu anataka ibada yetu itegemee kweli. Inasema hivi: “Wale wanaomwabudu [Mungu] lazima wamwabudu kwa roho na kweli.” (Yohana 4:24) Ili ujifunze jinsi kweli kutoka katika Biblia inavyoweza kukusaidia kutambua uwongo wa kidini na kujiepusha nao, soma mfululizo wa makala “Uwongo Unaofanya Watu Wasimpende Mungu.”

Kwa nini Mungu anataka mimi nijue kweli?

Mungu anataka upate wokovu, na unahitaji kujifunza ukweli kumhusu yeye ili ustahili kuokolewa. (1 Timotheo 2:4) Ukijifunza viwango vya Mungu kuhusu mema na mabaya na kuishi kupatana navyo, utakuwa na urafiki wa karibu pamoja naye. (Zaburi 15:1, 2) Mungu alimtuma Yesu duniani ili kuwasaidia watu wajifunze kweli. Mungu anataka tusikilize mafundisho ya Yesu.​—Mathayo 17:5; Yohana 18:37.

Je, Mungu atakomesha uwongo?

Ndiyo. Mungu anachukia watu wanapowalaghai wengine kwa kuwadanganya. Ameahidi kwamba atawaangamiza wale walioazimia kuendelea kusema uwongo. (Zaburi 5:6) Mungu atakapofanya hivyo, atatimiza ahadi yake inayosema hivi: “Midomo inayosema ukweli itadumu milele.”​—Methali 12:19.

Mistari ya Biblia kuhusu ukweli na kusema uwongo

Yohana 8:44: “[Ibilisi] ni mwongo na ndiye baba ya uwongo.”

Maana: Shetani Ibilisi alisema uwongo wa kwanza naye ndiye chanzo kikuu cha uwongo wote.

Methali 12:22: “Midomo inayosema uwongo humchukiza Yehova.”

Maana: Wale wanaompenda Mungu lazima wauchukie uwongo kama yeye anavyouchukia.

Yohana 4:24: “Wale wanaomwabudu [Mungu] lazima wamwabudu kwa roho na kweli.”

Maana: Mungu anataka ibada yetu ipatane na ukweli kumhusu yeye.

Yohana 8:32: “Kweli itawaweka ninyi huru.”

Maana: Ukweli ambao Yesu alifundisha unaweza kutuweka huru kutokana na ujinga, ushirikina, uwongo wa kidini, na mambo mengine mengi. Ona makala “‘Kweli Itawaweka Ninyi Huru’​—Jinsi Gani?”

1 Timotheo 2:4: “Mapenzi yake [Mungu] ni kwamba watu wa namna zote waokolewe na kupata ujuzi sahihi wa kweli.”

Maana: Mungu anataka tupate wokovu kwa kujifunza ukweli kumhusu.

a Yehova ni jina la kibinafsi la Mungu. (Zaburi 83:18) Ona makala “Yehova Ni Nani?”

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki