Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • ijwbq makala 32
  • Je, Biblia Inaweza Kunisaidia Nikishuka Moyo?

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Je, Biblia Inaweza Kunisaidia Nikishuka Moyo?
  • Maswali ya Biblia Yajibiwa
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • Jibu la Biblia
  • Msaada ambao Mungu huwapa walioshuka moyo
  • Msaada Kutoka kwa “Mungu wa Faraja”
    Amkeni!—2009
  • Unaweza Kuacha Kushuka Moyo
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1978
  • Faraja kwa Walioshuka Moyo
    Faraja kwa Walioshuka Moyo
  • “Mseme kwa Kuzifariji Nafsi Zilizoshuka Moyo”
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1983
Pata Habari Zaidi
Maswali ya Biblia Yajibiwa
ijwbq makala 32

Je, Biblia Inaweza Kunisaidia Nikishuka Moyo?

Jibu la Biblia

Ndiyo, kwa sababu msaada bora zaidi hutoka kwa “Mungu, Ambaye huwafariji na kuwatia moyo na kuwaburudisha na kuwachangamsha walioshuka moyo.”​—2 Wakorintho 7:6, The Amplified Bible.

Msaada ambao Mungu huwapa walioshuka moyo

  • Nguvu. Mungu ‘hukuburudisha na kukuchangamsha’ si kwa kuondoa matatizo yako, bali kwa kujibu sala zako unapoomba nguvu za kukabiliana na tatizo lako. (Wafilipi 4:13) Unaweza kuwa na uhakika kwamba yuko tayari kukusikiliza, kwa kuwa Biblia inasema: “Yehova yuko karibu na wale waliovunjika moyo; naye huwaokoa wale waliopondwa roho.” (Zaburi 34:18) Kwa kweli, Mungu anaweza kusikiliza sala zako za kuomba msaada hata ikiwa unashindwa kumweleza vizuri hisia zako.​—Waroma 8:26, 27.

  • Mifano mizuri. Mwandikaji mmoja wa Biblia alisali hivi kwa Mungu: “Toka upeo wa unyonge wangu, nakulilia, ee Mwenyezi-Mungu.” Mtunga-zaburi huyu alikabiliana na mshuko wa moyo kwa kukumbuka kwamba Mungu hataki tulemewe na hisia za hatia. Badala yake, alimwambia Mungu hivi: “Kama ee Mwenyezi-Mungu ungekumbuka maovu yetu nani ee Bwana, angeweza kusalimika? Lakini kwako twapata msamaha, ili sisi tukuheshimu.”​—Zaburi 130:1, 3, 4, Biblia Habari Njema.

  • Tumaini. Mbali na kutufariji sasa, Mungu ameahidi kuondoa matatizo yote yanayotufanya tushuke moyo. Wakati atakapotimiza ahadi hiyo, “mambo ya zamani [kutia ndani kushuka moyo] hayatakumbukwa akilini, wala hayataingia moyoni.”​—Isaya 65:17.

Taarifa: Ingawa Mashahidi wa Yehova wanakubali msaada ambao Mungu huandaa, wao pia hutafuta matibabu ya magonjwa kama vile kushuka moyo sana. (Marko 2:17) Hata hivyo, hatupendekezi matibabu yoyote hususa; kila mtu anapaswa kufanya uamuzi wake kuhusiana na matibabu.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki