Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • ijwyp makala 11
  • Ninawezaje Kuacha Kuahirisha Mambo?

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Ninawezaje Kuacha Kuahirisha Mambo?
  • Vijana Huuliza
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • Unahisi umelemewa na kazi fulani.
  • Huna kichocheo cha kufanya kazi hiyo.
  • Tayari una shughuli nyingi sana.
  • Uahirishaji—Mwizi wa Wakati
    Amkeni!—1995
  • Msaada wa Kuepuka Kuahirisha Mambo
    Daftari la Mkutano wa Huduma na Maisha Yetu ya Kikristo—2022
  • Ninaweza Kukabilianaje na Mkazo?
    Amkeni!—2012
  • Ninaweza Kutumiaje Vizuri Muda Wangu?
    Vijana Huuliza
Pata Habari Zaidi
Vijana Huuliza
ijwyp makala 11

VIJANA HUULIZA

Ninawezaje Kuacha Kuahirisha Mambo?

Je, umechoshwa na tabia yako ya kumaliza kazi za nyumbani na za shuleni ukiwa umechelewa? Kwa kweli unapaswa kuacha kuahirisha mambo! Makala hii itakusaidia uache kuahirisha mambo, hata kama

  • unahisi umelemewa na kazi fulani.

  • huna kichocheo cha kufanya kazi hiyo.

  • tayari una shughuli nyingi sana.

Baada ya kusoma makala hii, jibu maswali yetu kuhusu kuahirisha mambo.

Biblia inataja matokeo mabaya ya kuahirisha mambo. Inasema: “Anayeuangalia upepo hatapanda mbegu; naye anayetazama mawingu hatavuna.”—​Mhubiri 11:4.

Ona baadhi ya mambo yanayoweza kusababisha tatizo hilo na mambo unayoweza kufanya ili uache kuahirisha mambo.

Unahisi umelemewa na kazi fulani.

Ukweli wa mambo ni kwamba kazi fulani zinaonekana kuwa ngumu sana hivi kwamba inakuwa rahisi kuziahirisha. Yafuatayo ni madokezo machache yanayofaa.

  • Gawa mradi katika kazi ndogo-ndogo. “Hata nikijua nimechelewa kufanya jambo fulani, mimi hujaribu kufanya jambo moja kwa wakati mmoja,” anasema msichana anayeitwa Melissa.

  • Anza mara moja. “Anza kazi mara tu unapopewa, hata kama ni kuiandika tu katika orodha ya mambo unayopaswa kufanya au kuandika madokezo fulani kabla hujasahau.”​—Vera.

  • Omba msaada. Huenda wazazi au walimu wako wamekabili matatizo yale unayokabili. Unaweza kufaidika na ujuzi wao. Wanaweza kukusaidia kupanga mawazo yako na kuwa na ratiba.

Dokezo “Panga ratiba. Ni kweli kwamba hilo litamaanisha kupanga mambo na kuazimia kufuata ratiba hiyo, lakini utafaidika​—utatimiza mambo unayopaswa kutimiza kwa wakati wake.”​—Abbey.

Huna kichocheo cha kufanya kazi hiyo.

Mara nyingi, kazi ulizopewa zinatia ndani mambo ambayo hufurahii kabisa kufanya. Kwa hiyo, ufanye nini ikiwa kazi hiyo haikuvutii? Jaribu kufanya mambo yafuatayo.

  • Jitafutie sababu za kufanya kazi hiyo mapema. Kwa mfano, wazia jinsi utakavyohisi baada ya kukamilisha kazi hiyo. “Mimi hufurahi sana ninapokamilisha jambo kwa wakati au hata kabla ya wakati uliowekwa na ninaweza kustarehe,” anasema msichana anayeitwa Amy.

  • Jikumbushe kuhusu matokeo ya kuahirisha. Ukiahirisha jambo, unajiongezea mkazo na kujiharibia nafasi ya kufanikiwa. Biblia inasema: “Lolote lile analopanda mtu, atavuna hilo pia.”​—Wagalatia 6:​7.

  • Songeza karibu akilini mwako tarehe unayopaswa kuwa umemaliza. Msichana anayeitwa Alicia anasema hivi: “Mimi hufaidika ninapojiambia kwamba kazi inatakikana siku moja au mbili kabla ya tarehe yenyewe hususa. Ninaweza kuipitia tena na bado niwe na siku moja au mbili za ziada.”

Dokezo “Unaweza kutumia akili yako kama kichocheo. Jiambie kwamba utafanya yale unayopaswa kufanya na hakuna jambo lolote litakalokuzuia. Ninapojiambia hivyo, mimi hutimiza mambo yanayopaswa kufanywa.”​—Alexis.

Tayari una shughuli nyingi sana.

“Mara nyingi watu huniita mwahirishaji,” anasema mvulana anayeitwa Nathan, “lakini hilo si kweli! Hawajui kwamba mimi huwa na shughuli nyingi sana!” Ikiwa unahisi kama Nathan, jaribu kufuata madokezo yafuatayo.

  • Fanya kazi rahisi kwanza. Msichana anayeitwa Amber anasema hivi: “Mtu fulani aliniambia kwamba ikiwa kazi fulani itachukua muda wa chini ya dakika tano kuikamilisha, basi ifanye mara moja. Hilo linatia ndani kusafisha, kuanika nguo zako, kuosha vyombo, na kupiga simu.”

  • Panga mambo ya kutanguliza. Biblia inasema: “Mhakikishe mambo yaliyo ya maana zaidi.” (Wafilipi 1:10) Unawezaje kutumia andiko hilo katika maisha yako ya kila siku? Msichana anayeitwa Anna anasema: “Mimi huwa na orodha ya kazi zote ambazo ninapaswa kufanya na wakati zinapaswa kuwa zimekamilishwa. Lakini jambo muhimu zaidi ni kwamba mimi huandika ni lini nitaanza na kukamilisha kila kazi.”

Je, kufanya hivyo kunakuwekea vizuizi vingi? La, hasha! Ukweli wa mambo ni kwamba unapokuwa na ratiba, unadhibiti wakati wako badala ya kuruhusu wakati ukudhibiti. Hilo hupunguza mkazo. “Kuwa na ratiba hufanya nitulie na kujua mambo yaliyo ya muhimu zaidi,” anasema msichana anayeitwa Kelly.

  • Ondoa vikengeusha fikira. Jennifer anasema hivi: “Mimi humwambia kila mtu katika familia yetu ninapotaka kuanza kazi fulani ili kwamba ikiwa kuna jambo fulani wanataka nifanye waniambie kabla sijaanza kazi yangu. Pia mimi huzima simu yangu na vikumbusha vya kunijulisha kwamba nimepokea barua-pepe.”

Dokezo “Ikiwa kuna jambo lolote unalopaswa kufanya, lifanye, hakuna kazi inayoweza kujikamilisha yenyewe. Badala ya kufikiria kuhusu kazi hiyo kila wakati, mbona tu usiifanye ili ikuondokee? Ukiifanya, utatulia siku nzima.”​—Jordan..

Jibu maswali yetu kuhusu kuahirisha mambo.

Kweli au Si kweli

  1. Hupaswi kamwe kuchelewesha kazi yoyote.

  2. Watu walio na zoea la kuahirisha mambo wanaweza kubadilika.

  3. Unafanya kazi vizuri zaidi ukiwa chini ya mkazo.

  4. Ulirithi zoea la kuahirisha mambo kutoka kwa wazazi wako.

Majibu

  1. Si kweli. Huenda ukawa na sababu nzuri ya kuchelewesha kazi. Kwa mfano, huenda unahitaji wakati ili kupata habari zaidi, kupanga ratiba, au kufanya uamuzi unaofaa zaidi.​—Kanuni ya Biblia: Methali 21:5.

  2. Kweli. Unaweza kuacha mazoea mabaya. Siri ni kukazia fikira faida za kubadili mazoea hayo.​—Kanuni ya Biblia: Waefeso 4:​22, 23.

  3. Si kweli. Mara nyingi huwezi kufanya kazi vizuri chini ya mkazo. Ukweli ni kwamba unafanya kazi vizuri zaidi ikiwa una wakati wa kutosha na umepanga mambo kimbele.​—Kanuni ya Biblia: Methali 15:28.

  4. Si kweli. Hata ikiwa mmoja wa wazazi wako ana mwelekeo wa kuahirisha mambo, hakuna uthibitisho wowote unaoonyesha kwamba unaweza kurithi zoea hilo.”​—Kanuni ya Biblia: Wagalatia 6:5.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki