Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • ijwbq makala 62
  • Ninawezaje Kujilinda Dhidi ya Kusumbuliwa Kingono?

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Ninawezaje Kujilinda Dhidi ya Kusumbuliwa Kingono?
  • Maswali ya Biblia Yajibiwa
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • Jibu la Biblia
  • Naweza Kupambanaje na Kusumbuliwa Kingono?
    Amkeni!—2000
  • Kusumbuliwa Kingono—Jinsi Unavyoweza Kujikinga
    Amkeni!—1996
  • Nifanye Nini Nikisumbuliwa Kingono?
    Vijana Huuliza
  • Kusumbuliwa Kingono—Tatizo la Duniani Pote
    Amkeni!—1996
Pata Habari Zaidi
Maswali ya Biblia Yajibiwa
ijwbq makala 62

Ninawezaje Kujilinda Dhidi ya Kusumbuliwa Kingono?

Jibu la Biblia

Fikiria mapendekezo haya yanayotegemeka na yanayopatana na hekima ya Biblia:

  1. Kazia fikira kazi yako. Pendezwa na kuwaheshimu wafanyakazi wenzako, lakini usiruhusu urafiki ambao unaweza kuwafanya wafikiri unapendezwa nao kimapenzi.​—Mathayo 10:16; Wakolosai 4:6.

  2. Valia kwa kiasi. Kuvaa nguo zinazoamsha ashiki kutafanya wengine watuelewe vibaya. Biblia inatutia moyo tuvalie kwa “kiasi na utimamu wa akili.”​—1 Timotheo 2:9.

  3. Chagua marafiki wako kwa hekima. Ikiwa unatumia wakati mwingi pamoja na wale ambao wanapenda kuchezewa kimapenzi, ni rahisi kutendewa kama wao.​—Methali 13:20.

  4. Epuka mazungumzo machafu. Usijihusishe kwenye mazungumzo yenye ‘hadithi chafu, au mizaha kuhusu ngono’.​—Waefeso 5:4.

  5. Epuka vishawishi. Kwa mfano, uwe mwangalifu kuhusu mialiko ya kubaki kazini baada ya muda wa kazi ikiwa si lazima​—Methali 22:3.

  6. Uwe imara na useme waziwazi. Ikiwa unasumbuliwa kingono, mweleze waziwazi mtu huyo kwamba hupendi tabia yake. (1 Wakorintho 14:9) Kwa mfano, unaweza kusema hivi: “Unanishika-shika, na sipendi tabia hiyo. Usiniguse.” Unaweza kumwandikia barua na kumweleza kilichotokea, jinsi ulivyohisi na kwamba hutaki arudie tena. Sema waziwazi kwamba msimamo wako unategemea maadili na mambo unayoamini.​—1 Wathesalonike 4:​3-5.

  7. Tafuta msaada. Ikiwa unaendelea kusumbuliwa kingono, mweleze rafiki yako unayemwamini, mshiriki wa familia, mfanyakazi mwenzako au mtu mwenye uzoefu wa kusaidia watu wenye tatizo kama lako. (Methali 27:9) Waathiriwa wengi wamepata msaada kupitia sala. Hata kama hujawahi kusali, usipuuze msaada unaoweza kupata kutoka kwa Yehova “Mungu wa faraja yote.”​—2 Wakorintho 1:3.

Kusumbuliwa kingono hufanya mazingira ya kazi kuwa yenye kuogopesha kwa watu wengi, hata hivyo Biblia inaweza kutusaidia.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki