Je, Wafuasi Wenu
Ndiyo. Mashahidi wote wa Yehova ni wahubiri, au wahudumu—kutia ndani mamilioni ya wanawake ambao ni Mashahidi. Kama Biblia ilivyotabiri, “wanawake wanaotangaza habari njema ni jeshi kubwa.”—Zaburi 68:11.
Wanawake ambao ni Mashahidi wa Yehova hufuata mfano wa wanawake wanaotajwa katika Biblia. (Methali 31:10-31) Ingawa wao si viongozi katika kutaniko, wanashiriki kikamili katika kazi ya kuwahubiria watu. Wao pia huwafundisha watoto wao kanuni za Biblia. (Methali 1:8) Kwa maneno na matendo, wanawake ambao ni Mashahidi huwawekea wengine mfano mzuri.—Tito 2:3-5.