Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • ijwyp makala 43
  • Nawezaje Kupatana na Wazazi Wangu?

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Nawezaje Kupatana na Wazazi Wangu?
  • Vijana Huuliza
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • Maswali kuhusu mizozo
  • Kwa nini mizozo hutokea
  • Unaweza kufanya nini
  • Kufurahisha Mioyo ya Wazazi Wako
    Kufanya Maisha ya Jamaa Yako Yawe Yenye Furaha
  • Nifanye Nini Wazazi Wangu Wanapogombana?
    Maswali Ambayo Vijana Huuliza—Majibu Yafanyayo Kazi, Buku la 2
  • Ninawezaje Kuwafahamu Wazazi Wangu Vizuri Zaidi?
    Amkeni!—2009
  • Kwa Nini Kuna Sheria Nyingi Sana?
    Maswali Ambayo Vijana Huuliza—Majibu Yafanyayo Kazi, Buku la 2
Pata Habari Zaidi
Vijana Huuliza
ijwyp makala 43
Watoto wakifurahia mazungumzo pamoja na wazazi wao wakitembea kwenye bustani

VIJANA HUULIZA

Nawezaje Kupatana na Wazazi Wangu?

  • Maswali kuhusu mizozo

  • Kwa nini mizozo hutokea

  • Unaweza kufanya nini

  • Vijana wenzako wanasema nini

Maswali kuhusu mizozo

  • Ni mzazi yupi ambaye wewe huzozana naye kwa urahisi?

    • Baba

    • Mama

  • Mnazozana mara nyingi kadiri gani?

    • Mara chache

    • Baada ya muda fulani

    • Mara nyingi

  • Mzozo huo unakuwa mkubwa kadiri gani?

    • Unasuluhishwa haraka na kwa amani.

    • Utasuluhishwa lakini baada ya kubishana sana.

    • Hatusuluhishi chochote​—hata baada ya kubishana sana.

Ikiwa hampatani na wazazi wako, huenda ukajiambia kwamba wao wanapaswa kufanya jambo fulani ili kuboresha hali. Hata hivyo, kama tutakavyoona, kuna mambo ambayo wewe unaweza kufanya ili kupunguza mabishano na mizozo. Kwanza, fikiria . . .

Kwa nini mizozo hutokea

  • Uwezo wa kufikiri. Unapoendelea kukua, unaanza kufikiria mambo kwa uzito zaidi kuliko ulivyokuwa ukifikiri ulipokuwa mtoto. Unaanza pia kufanya maamuzi thabiti​—na huenda baadhi ya maamuzi hayo yakapingana na maamuzi ya wazazi wako. Hata hivyo, Biblia inasema hivi: “Mheshimu baba yako na mama yako.”​—Kutoka 20:12.

    Ukweli wa mambo: Ukomavu na ustadi unahitajika ili hata usipokubaliana na jambo usikosane na watu.

  • Uhuru. Unavyoendelea kukomaa, wazazi wako watakupa uhuru zaidi. Tatizo ni kwamba huenda usiwe na uhuru mwingi kadiri unavyotaka au wakati unapoutaka​—na hilo linaweza kusababisha mzozo. Hata hivyo, Biblia inasema hivi: “Enyi watoto, watiini wazazi wenu.”​—Waefeso 6:1.

    Ukweli wa mambo: Mara nyingi, kiasi cha uhuru ambacho wazazi watakupa kinategemea jinsi unavyotumia uhuru ambao tayari wamekupa.

Unaweza kufanya nini

  • Zingatia jukumu lako. Badala ya kuwalaumu wazazi wako kwa sababu ya mzozo uliopo kati yenu, fikiria mambo unayoweza kufanya ili kuwe na amani. Kijana anayeitwa Jeffrey, anasema hivi: “Mara nyingi si kile wazazi wanachosema kinachosababisha mzozo, ni jinsi unavyoitikia. Kuzungumza kwa utulivu huchangia sehemu kubwa katika kuleta amani.”

    Biblia inasema hivi: “Kwa kadiri inavyowategemea ninyi, iweni wenye kufanya amani.”​—Waroma 12:18.

  • Sikiliza. Samantha, mwenye umri wa miaka 17, anasema hivi: “Naona hilo ndilo jambo gumu zaidi kwangu kufanya. Lakini nimetambua kwamba wazazi wanapoona kwamba unasikiliza, watakusikiliza pia.”

    Biblia inasema hivi: ‘Uwe mwepesi kuhusu kusikia, si mwepesi wa kusema.’​—Yakobo 1:19.

    1. Sufuria ikiwaka moto ikiwa jikoni; 2. Moto ukiwa umevuka mipaka

    Mzozo ni kama moto​—usipodhibitiwa, unaweza kuvuka mipaka

  • Kumbuka mko upande mmoja. Ona mzozo kama mchezo, kama vile shindano la tenisi. Wazia kwamba wewe na wazazi wako mko upande mmoja, na jambo mnalozozania liko upande ule mwingine. Mwanamume kijana anayeitwa Adam anasema hivi: “Kunapokuwa na mzozo, wazazi humtakia tineja kile wanachoona kuwa kinamfaa naye tineja hutaka kile anachofikiri kuwa kinafaa. Hivyo, kihalisi wote wana kusudi moja.”

    Biblia inasema hivi: “Tufuatilie mambo yanayofanya kuwe na amani.”​—Waroma 14:19.

  • Elewa hali. Tineja anayeitwa Sarah, anasema hivi: “Inanisaidia kukumbuka kwamba wazazi pia wana matatizo wanayokabiliana nayo, ambayo ni makubwa tu kama yetu.” Msichana anayeitwa Carla, anaongezea hivi: “Mimi hujiwazia nikiwa mzazi. Ningefanyaje ikiwa ningekuwa nalea mtoto na kushughulika na hali sawa na hiyo? Ningefanya nini ambacho kingemnufaisha mtoto wangu?”

    Biblia inasema hivi: “Mkiendelea kuangalia, si faida za kibinafsi za mambo yenu wenyewe tu, bali pia faida za kibinafsi za wengine.”​—Wafilipi 2:4.

  • Uwe mtiifu. Kwa ujumla, Biblia inasema ufanye hivyo. (Wakolosai 3:​20) Na mambo yatakuwa rahisi zaidi ikiwa utafanya hivyo. Msichana anayeitwa Karen, anasema hivi: “Ninapunguza mkazo maishani ninapofanya kile ambacho wazazi wananiambia nifanye. Tayari wamefanya mengi kwa niaba yangu, hilo ni jambo dogo ambalo wanastahili kutoka kwangu.” Mojawapo ya njia bora zaidi za kusuluhisha mizozo ni kutii!

    Biblia inasema hivi: “Pasipo na kuni moto huzimika.”​—Methali 26:20.

Dokezo. Ikiwa ni vigumu kwako kueleza hisia zako, jaribu kuandika mawazo yako kwenye karatasi au kwenye ujumbe mfupi. Tineja anayeitwa Alyssa, anasema hivi: “Mimi hufanya hivyo ikiwa siko katika hali nzuri kiakili kuzungumza. Hilo hunisaidia kujieleza bila kupiga kelele au kusema jambo ambalo nitajutia baadaye.”

VIJANA WENZAKO WANASEMA NINI

Marilyn

“Kila mtu anapokuwa amechoka, ni vigumu kudhibiti hisia anaposhughulikia tatizo fulani. Nyakati nyingine jambo linalofaa zaidi ni kuacha kulizungumzia, kukumbatiana, na kwenda kulala. Hisia huwa zimetulia kufikia asubuhi.”​—Marilyn.

Devin

“Ukiwa na subira unaweza kukabiliana na hali yoyote. Mzozo unapokaribia kuanza, nyamaza, utulie, na kufikiri. Matatizo hutokea mtu anapoendelea kuzungumza bila kufikiri.”​—Devin.

Mackenzie

“Singependa kujuta baadaye kwamba sikuwatendea wazazi wangu kwa njia inayofaa. Hilo hunisaidia kuwasikiliza na kutochukua mambo madogo kwa uzito kupita kiasi.”​—Mackenzie.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki