Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • ijwyp makala 57
  • Kwa Nini Nifanye Amani na Ndugu na Dada Zangu?

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Kwa Nini Nifanye Amani na Ndugu na Dada Zangu?
  • Vijana Huuliza
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • Marafiki wa karibu zaidi wanaokasirishana zaidi
  • Sababu mbili za kufanya amani
  • Nifanye Nini ili Nielewane na Ndugu na Dada Zangu?
    Amkeni!—2010
  • Nawezaje Kuwa Kiolezo kwa Ndugu na Dada Zangu Wachanga?
    Amkeni!—1992
  • Nifanye Nini ili Nielewane na Ndugu na Dada Zangu?
    Maswali Ambayo Vijana Huuliza—Majibu Yafanyayo Kazi, Buku la 1
  • Kwa Nini Mimi Niwe Ndiye Kitindamimba?
    Amkeni!—1992
Pata Habari Zaidi
Vijana Huuliza
ijwyp makala 57
Ndugu na dada yake wakitengeneza piza pamoja

VIJANA HUULIZA

Kwa Nini Nifanye Amani na Ndugu na Dada Zangu?

  • Marafiki wa karibu zaidi wanaokasirishana zaidi

  • Sababu mbili za kufanya amani

  • Vijana wenzako wanasema nini

Marafiki wa karibu zaidi wanaokasirishana zaidi

Inasemekana kwamba watoto wa familia moja ndio marafiki wa karibu zaidi wanaokasirishana zaidi. Unawapenda ndugu na dada zako, nao wanakupenda​—lakini nyakati fulani unaona ni vigumu kuelewana nao. Helena mwenye umri wa miaka 18 anasema hivi: “Ndugu yangu mdogo huniudhi sana, anajua ni mambo gani yanayoniudhi na ni wakati gani nitakasirika akiyafanya!”

Baadhi ya ugomvi kati ya watoto wa familia moja unaweza kusuluhishwa kwa kujadiliana na kufikia mwafaka. Kwa mfano:

  • Ndugu wawili wanaoishi kwenye chumba kimoja wanaweza kubishana kwa sababu kila mmoja anataka faragha. Suluhisho ni nini? Wanahitaji kujifunza kusikilizana na kuruhusu kila mmoja awe na faragha. Tumia kanuni ya Biblia inayopatikana kwenye Luka 6:​31.

  • Akina dada wawili wanaweza kuwa na kawaida ya kuvaa nguo za mwenzake bila kuomba. Suluhisho ni nini? Wanapaswa kuzungumzia jambo hilo na kuweka mipaka inayofaa. Tumia kanuni ya Biblia inayopatikana kwenye 2 Timotheo 2:​24.

Katika visa vingine, matatizo kati ya ndugu au dada yanaweza kuwa mazito sana na kusababisha matokeo mabaya. Fikiria mifano miwili ya Biblia:

  • Miriamu na Haruni walimwonea wivu Musa ndugu yao, na matokeo yalikuwa yenye kuhuzunisha. Soma simulizi hilo kwenye Hesabu 12:​1-​15. Kisha jiulize hivi: ‘Ninawezaje kuepuka kumwonea wivu ndugu au dada yangu?’

  • Kaini alipandwa na hasira hivi kwamba akamuua Abeli, ndugu yake. Soma simulizi hilo kwenye Mwanzo 4:​1-​12. Kisha jiulize hivi: ‘Ninawezaje kudhibiti hasira yangu ninaposhughulika na ndugu au dada yangu?’

Sababu mbili za kufanya amani

Hata kama si rahisi kusuluhisha ugomvi kati yako na ndugu au dada zako, kuna angalau sababu mbili zinazoonyesha kwa nini ujitahidi kufanya hivyo.

  1. Ni ishara ya ukomavu. “Nilikuwa nikikasirika haraka niliposhughulika na dada zangu wawili wadogo,” anasema kijana anayeitwa Alex. “Sasa nimekuwa mtulivu na mwenye subira ninaposhughulika nao. Unaweza kusema kwamba sasa nimekomaa.”

    Biblia inasema hivi: “Yule ambaye si mwepesi wa hasira ana utambuzi mwingi, lakini anayekosa subira anainua upumbavu.”​—Methali 14:29.

  2. Ni mazoezi mazuri kwa ajili ya wakati ujao. Ikiwa huwezi kuvumilia kutokamilika kwa ndugu au dada zako, utawezaje kushirikiana na mwenzi wako, mfanyakazi mwenzako, mwajiri wako, au mtu mwingine unayekutana naye?

    Ukweli wa maisha: Mafanikio yako ya wakati ujao katika mahusiano na wengine yanategemea uwezo wa kuwasiliana na kujadili jambo, na hakuna mahali panapofaa pa kusitawisha ujuzi huo kama unaposhughulika na watu wa familia yako.

    Biblia inasema hivi: “Kwa kadiri inavyowategemea ninyi, iweni wenye kufanya amani na watu wote.”​—Waroma 12:18.

Ungependa kupata msaada wa kusuluhisha matatizo na ndugu au dada yako? Soma “Vijana Wenzako Wanasema Nini,” kisha ungalie daftari linalohusiana na habari hii lenye kichwa, “Kuwa na Uhusiano Mzuri na Ndugu au Dada Zangu.”

Vijana Wenzako Wanasema Nini

Jessica

“Nina dada watatu, na ninaweza kusema kwamba si rahisi sikuzote kudumisha uhusiano mzuri pamoja nao. Lakini pia, nimegundua kwamba wao ndio wanaonijua vizuri na sikuzote watanisaidia nitakapohitaji msaada.”​—Jessica.

Tyler

“Kuna wakati ambapo ninamkasirisha ndugu yangu au yeye ananikasirisha. Ninampenda sana ndugu yangu. Yeye ndiye mtu ambaye mara nyingi ananifanya nijiamini zaidi. Ninapenda sana udumifu wake​—hakati tamaa na kila mara anafanya mengi zaidi ya yale anayopaswa kufanya.”​—Tyler.

Cameo

“Ninapenda kuwa pamoja na watu wengine, kwa hiyo kuwa na ndugu wadogo wawili ni jambo bora kwangu. Kwa kuwa wao ni wadogo, kuwa pamoja nao kunanifundisha mambo mengi kuhusu jinsi ya kushughulika na watu wenye umri tofauti na wangu. Ninathamini sana kuwa na ndugu hao.”​—Cameo.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki